• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AZIDI KUWAJAZIA MAPESA PAMBA JIJI FC SASA KILA GOLI ANUNUA KWA MILIONI MOJA

Posted on: March 27th, 2024

RC MAKALLA AZIDI KUWAJAZIA MAPESA  PAMBA JIJI FC SASA KILA GOLI ANUNUA KWA MILIONI MOJA


*Awapongeza matokeo ya mchezo wa ugenini dhidi ya Kengold*


*Awataka kukaza buti michezo minne iliyosalia*


*Awasihi kuepuka kurubuniwa na kusaliti timu*


Wakati filimbi ya kuhitimishwa michuano ya ligi ya Championship ikiwa ukingoni kupulizwa, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amezidi kuwapa ari wachezaji wa timu ya Pamba Jiji FC kwa kununua kila GOLI Sh. Milioni moja kwa michezo yao minne iliyosalia.

Makalla ambaye ni mlezi wa timu hiyo amesema hayo leo Machi 27, 2024 alipowatembelea wachezaji wa Pamba Jiji kwenye uwanja mkongwe wa Nyamagana, amesema mbali ya motisha hiyo pia amewapa Sh. Milioni 5.2 kama bonus yao kutokana na mwenendo mzuri na kucheza soka la kiwango hasa katika mpambano wa ugenini dhidi ya Kengold.

"Mimi sina maneno mengi zaidi ya kuwa mtu wa vitendo kama nilivyowaahidi,ule mchezo dhidi ya Kengold mliwafanya wenyeji wenu kama wapo ugenini kutokana na soka mliowatandazia na mwishowe tukatoka share ya 2-2 na kupata alama moja ambayo imetuweka pazuri", CPA Makalla.

Makalla ambaye ni mkereketwa wa soka ametaka Pamba Jiji FC kuwa na juhudi zaidi uwanjani kwa kufunga mabao mengi na hatakuwa na hiana kwenye kutoa fungu la pesa la magoli hayo  na kuwasisitiza kutokubali kuruhusu mabao ya kufungwa.

"Hapa naomba tuelewane mkishinda 3-2 hapo natoa milioni moja tu kutokana na kuruhusu magoli mengi ya kufungwa,safu ya ulinzi na mabeki nataka kuona ukatili wa kutoruhusu mpinzani kuwapenya na kuwafunga," amehimiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Katika mazungumzo hayo na wachezaji Makalla amewataka kutanguliza uzalendo na kutokubali kurubuniwa hasa kwa kipindi hiki cha michuano kuelekea ukingoni kutokana na timu zilizowakaribia kuweza kufanya fitna ili zipate nafasi.

Nahodha wa timu hiyo na mchezaji mkongwe Jerryson Tegete amemuhakikishia mlezi wao sasa wachezaji wote wsmeshaona njia nyeupe ya kucheza ligi kuu nsimu ujao,hivyo wataendelea kuzingatia maelekezo yote kuanzia kwake na dawati lao la ufundi.

Timu ya soka ya Pamba Jiji FC hadi sasa imejikusanyia kibindoni point 55 baada ya kucheza michezo 26 na kushika nafasi ya pili nyuma wa vinara wa kundi hilo Kengold wenye pointing 60 na Jumamosi watawaalika Polisi Tanzania mpambano utakaorindima kwenye uwanja wa Nyamagana.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti