• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AZINDUA RASMI USIKILIZAJI WA KERO ZA WANANCHI MWANZA

Posted on: September 18th, 2023

RC MAKALLA AZINDUA RASMI USIKILIZAJI WA KERO ZA WANANCHI MWANZA


*Aagiza kwa wakuu wa Wilaya kila siku ya alhamisi iwe ya kusikiliza kero za wananchi


*Atoa agizo kwa Maafisa kutoa ushauri wa kisheria mapema kwa wananchi kabla ya shauri kufikishwa Mahakamani*


*Awataka watumishi kuwa na uwajibikaji wenye tija wa kusikiliza na kutoa maamuzi  kero za wananchi


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA. Amos Makalla leo Septemba 18, 2023 amezindua rasmi zoezi la kusikiliza kero za wananchi Mkoani humo na ametoa maagizo kwa wakuu wa Wilaya kila siku ya alhamisi iwe ya kusikiliza kero za wananchi kwa kuwasikiliza na kutoa maamuzi

Akizindua kampeni hiyo kwenye viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa akiambatama na Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na viongozi wa taasisi mbalimbali za Serikali CPA Makalla amebainisha utaratibu huo ulkifanyika kikamilifu utaondoa kero nyingi za wananchi na kutowafikia viongozi wa juu wanapokuja kuwatembelea maeneo yao.

"Nimeunda kikosi kazi cha kuzungukia Wilaya zote kupokea taarifa za migogoro ya ardhi lakini niwahimize maafisa ardhi  toeni mapema ushauri wa kisheria kwa wananchi hali itakayowasaidia kupata haki zao mapema," amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Ameongeza kuwa kumekuwa na kero kubwa kwa wananchi hasa eneo la ardhi ambapo idadi kubwa wamekuwa wakipoteza haki zao kutoka kwa baadhi ya watu wenye uwezo ambao wamekuwa wakikimbilia mahakamani na kushinda mashauri husika kutokana na wananchi kushindwa kupata tafsiri vizuri za kisheria na kujikuta wakipoteza haki zao.

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa ufafanuzi usikilizaji wa kero hizo siyo kwa mashauri ambayo tayari yametinga mahakamani kwani kisheria hana mamlaka ya kuingilia mhimili huo,hivyo amewataka wananchi kuwasilisha matatizo yao ambayo hayajafika kwenye vyombo vya sheria.

"Leo nafanya uzinduzi huu nikiamini mmepata somo la kujifunza namna ya kushughulikia kero za wananchi, sitarajii nikifika kwenye Halmashauri zenu nikute idadi kubwa ya wananchi wenye kero na badala yake mkafanye kazi hii kwa umakini na utatuzi haraka",amesisitiza CPA Makalla kwa viongozi.

Katika uzinduzi huo wa kusikiliza kero za wananchi kutoka Wilaya za Nyamagana na Ilemela,wananchi wengi waliojitokeza walikuwa na kero za ardhi ambazo baadhi mashauri tayari yalikuwa mahakamani na kero zingine Mkuu huyo alizipatia ufumbuzi hapo hapo.

Baada ya uzinduzi huo Wakuu wa Wilaya wote kutoka Mkoani Mwanza wataendelea na zoezi hilo kwenye vituo vyao kwa kujipangia utaratibu wa siku za kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi kuanzia kwenye ngazi za vitongoji.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti