• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AZITAKA HALMASHAURI KUKAMILISHA MIUNDOMBINU YA MADARASA ILI KUPOKEA WANAFUNZI 2024

Posted on: December 19th, 2023

RC MAKALLA AZITAKA HALMASHAURI KUKAMILISHA MIUNDOMBINU YA MADARASA ILI KUPOKEA WANAFUNZI 2024


*Amezitaka Halmashauri kukamilisha ujenzi madarasa ya awali, Msingi na Sekondari*


*Aagiza kamati za isalama na watendaji kushirikiana kukomesha utoro na watoto kuanza shule mara moja*


*Awataka waratibu elimu wa kata kusimamia kuboresha ubora wa elimu*


*Awapongeza walimu na viongozi wote kwa kupandisha ufaulu darasa la saba*


*Awataka viongozi kuhamasisha wazazi ili kuwa na programu ya chakula kwa wanafunzi shuleni*


*Awataka watendaji kutumia taasisi za elimu kupata maoni ya uboreshaji wa sekta*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka viongozi kwenye wilaya zote mkoani humo kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya madarasa, mabweni na matundu ya vyoo hadi kufikia mwanzo wa muhula mpya wa masomo mwezi januari 2024 ili kuwa tayari kupokea wanafunzi.

CPA Makalla amesema hayo mapema leo Jumanne ya 19 Disemba, 2023 wakati wa kikao kazi cha wadau wa elimu kilichokutana mahsusi kuweka mikakati ya kupokea watoto wanaojiunga na shule za awali, msingi na sekondari ndani ya Mkoa wa Mwanza hususani ukamilishaji wa ujenzi wa miundombinu ya madarasa.


Amesema halmashauri zinapaswa kukamilisha miundombinu ya madarasa ipasavyo kama Serikali ilivyoagiza ili kutoa nafasi kwa watoto waliofikia umri wa kujiunga na shule za awali na waliofaulu kwenda sekondari waweze kujiunga mara moja na kwenye hilo kamati za usalama na watendaji lazima washirikiane pamoja na kukomesha utoro kwa wanafunzi.

"Sitarajii kusikia mtumishi au kiongozi wa Sengerema anakula sikukuu sehemu fulani ndani ya huu muda wakati mpo asilimia 45 tu ya utekelezaji wa agizo la kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya elimu, fanyeni kazi usiku na mchana harakisheni kazi hii ili mtoke mlipo na ifikapo mwanzo wa muhula muweze kupokea watoto." Mkuu wa Mkoa.

Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza Martine Nkwabi amefafanua kuwa jumla ya shule za Msingi 991 za Mkoa huo zilifanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi 2023  kwa watahiniwa 92, 655 ambapo watahiniwa 78, 437 ikiwa ni asilimia 84.7 (wavulana 36,397 na wasichana 42,040) wamefaulu na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza Januari 2024.


"Matokeo yameonesha asilimia ya ufaulu wa Mkoa imepanda kutoka asilimia 82.63 ya mwaka 2022 hadi 84.72 sawa na ongezeko la asilimia 2.09 na ongezeko hilo limetokana na Halmashauri zote 7 kupandisha ufaulu ikiongozwa na Halmazhauri ya Misungwi iliyopanda kwa asilimia 5 japokua ni ya mwisho kimkoa kwa ufaulu" Amesema Afisa Elimu.

Ameongeza kuwa pamoja na uwepo wa miundombinu na vifaa bora shuleni bado watendaji wa kata, vijiji na mitaa wana nafasi ya kuhamasisha wazazi kupeleka watoto shule na kuona namna ya kusaidia kuwepo kwa programu ya chakula shuleni ili kuthibiti utoro shuleni na kwenye suala hilo ameitaja Mwanza kuwa nafasi ya 21 kama Mkoa kutoa chakula shuleni.

Awali, Afisa Elimu awali na msingi Jiji la Mwanza, Mwalimu Musa Langwe akijibu tuhuma za Halmashauri hiyo kuwa na msongamano wa wanafunzi amebainisha kuwa shule ya Nyerere na zingine ndani ya Halmashauri hiyo wana upungufu wa zaidi ya madarasa elfu 1 lakini wanaendelea na ujenzi wa madarasa 3 kwenye shule hiyo na zingine ili kukabiliana na tatizo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti