• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC Malima ahimiza kukamilika kwa wakati na ujenzi bora wa madarasa na Ofisi za walimu Mkoani Mwanza

Posted on: December 18th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima leo amefanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa madarasa akianzia Wilaya za Nyamagana,Ilemela na Magu na kuhimiza ujenzi bora na kumalizika kwa wakati kabla ya mwaka huu kumalizika.

Mkuu huyo wa Mkoa akianzia ziara hiyo Wilayani Nyamagana shule ya Sekondari Mirongo amekagua ujenzi wa madarasa ya maghorofa na kutaka ofisi za walimu zisiwe mbali na madarasa hayo ili kudumisha nidhamu kwa wanafunzi na uwepo mzuri wa uwiano wa matundu ya vyoo na idadi ya wanafunzi.

"Noana maendeleo mazuri ya ujenzi wa madarasa lakini hili la ofisi za walimu kuwa mbali sijafurahishwa nalo kabisa,kila baada ya madarasa matatu lazime iwepo ofisi ya walimu ndiyo ujenzi wa kisasa ninao utaka" Mhe.Malima

"Wilaya ya Nyamagana tumepokea Shs Bilioni 3.92 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 196,ambapo 130 yatakuwa ya chini na 60 ya ghorofa na madarasa yote yapo hatua za mwisho kukamilika kabla ya Disemba hii,tunatarajia kuwapokea Januari mwakani wanafunzi wote waliofaulu mwaka huu" Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe Amina Makilagi.

Aidha Mhe Malima akiwa Wilayani Nyamagana amekagua mradi wa barabara ya Unguja A ya mita 372 iliyogharimu Shs milioni 295 chini ya Mkandarasi Nyanza Road Works ambayo utekelezaji wake umefikia asilimia 73 ukigharimiwa na mfuko wa barabara

"Sisi Wilaya ya Ilemela tumepokea Shs Bilioni 2.2 za ujenzi wa madarasa 110,tayari 88 yamekamilika na 22 yapo hatua ya ukamilishaji,mahitaji yalikuwa madarasa 252 lakini tumejenga jumla 2548"Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ilemela Injinia Modest Apolinary.

Huko Wilayani Magu Mhe.Malima amefanya ukaguzi wa barabara ya Kisesa-Bujora yenye urefu wa Kilomota 1.72 inayojengwa na Mkandarasi Mangi Construction Ltd Kwa gharama ya zaidi ya Shs Bilioni 1 iliyo chini ya TARURA lakini inakabiliwa na changamoto ya uwepo wa mawe makubwa ardhini na kusua sua kwa kuondolewa nguzo za Tanesco na minara ya Kampuni za simu.

"Mmeniambia hii barabara mnatarajia kunikabidhi Mei 6 mwakani,sasa hizi changamoto nataka kesho mzizungumze kwa kina kikao cha bodi ya barabara ili nami nijue eneo langu kama Mkuu wa Mkoa nazitatuaje" amesisitiza Mkuu wa Mkoa

"Tumepokea zaidi ya Shs Bilioni 1 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 163 ujenzi upo hatua ya asimia 82 na madarasa 26 yapo hatua ya ukamilishaji na mengine yamekamilika tunatarajia Disemba 22 mwaka huu madarasa yote kuwa tayari"Mkurugenzi wa Halmashauri ya Magu Fidelica Myoveka.

Mkoa wa Mwanza umepokea zaidi ya Shs Bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa Wilaya zote zilizopo ndani ya Mkoa huo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti