• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC Malima ahimiza Sensa ya Watu na Makazi Mwanza

Posted on: August 4th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima amewataka viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza kuweka mkazo kwenye zoezi la Sensa ya watu na Makazi linayotarajia kufanyika jumanne ya Agosti 23, 2022 nchini ili lifanikiwe kwa kiwango kilichokusudiwa.

Mhe. Malima amesema hayo  Agosti 03, 2022 wakati akizungumza na Viongozi, watumishi na wadau wa maendeleo wilayani  Nyamagana akiwa kwenye ziara ya kujitambulisha na kupata taarifa ya Maendeleo kufuatia kuteuliwa kwake kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza mwishoni mwa wiki.

Aidha, Mhe Malima amesema amefurahishwa na mwenendo wa Ukusanyaji wa mapato ya ndani kwenye Halmashauri hiyo na ametoa wito kwa Watumishi kuhakikisha wanaongeza wigo wa Ukusanyaji wa mapato na kuboresha upatikanaji wa huduma bora kwa jamii kama vofaa tiba kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya.

"Wananchi wa Nyamagana wamewakabidhi hatma ya maisha yao, nendeni mkaonekane kwenye Ukusanyaji wa Mapato, utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kupunguza hoja za mdhibiti na mkaguzi wa Hesabu za Serikali maana mimi nachukia sana kuwepo kwa hoja za kizembe kutokana na kutokujali." Mhe. Malima.

Aidha, ameagiza kupatiwa taarifa ya utekelezaji wa zoezi la mikopo ya asilimia kumi kwa makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kutoka sehemu ya Ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri kwani ni kiu yake kuona usimamizi wa dhati kwenye eneo hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amesema Ukusanyaji wa Mapato 2021/22 Halmashauri ya Jiji la Mwanza wamekusanya Zaidi ya Bilioni 18 sawa na Asilimia 103 ya makisio na wamekua wakitekeleza Miradi kadhaa ya kimkakati ukiwemo Mradi wa Stendi ya kisasa ya Nyegezi inayotekelezwa kwa Bilioni 23 ikiwa imefikia 76 ya utekelezaji.

Aidha, amesema Wilaya hiyo kupitia Halmashauri ya Jiji imekua ikitekeleza kwa dhati miradi mbalimbali ya Maendeleo katika sekta za Elimu, Afya, Uvuvi, Ufugaji na Miundombinu ambako kote wamekua mstari wa mbele kuimarisha jamii kwa kuwajengea uwezo katika shughuli wanazofanya.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti