• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC Malima aikumbusha FEMATA kutunza Mazingira nchini

Posted on: May 5th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amelipongeza Shirikisho la Wachimba Madini nchini FEMATA kwa kupiga hatua na kutoa mchango kwenye Pato la Taifa na kuwakumbusha kutanguliza maslahi ya nchi kwa kuzingatia utunzaji wa Mazingira.

Akizungumza na uongozi na wanachama wa Shirikisho hilo kwenye ufunguzi wa wiki ya Madini inayofanyika kwenye viwanja vya Rock City Mall Jijini Mwanza,Mkuu huyo wa Mkoa amesema anashuhudia mabadiliko ya wachimbaji wadogo hapa nchini kuanzia kwenye vifaa,ajira,kuelimika na mshikamano uliopo miongoni mwao ambao umekuwa na tija kwa maendeleo ya Taifa.


"Bwana Rais wa FEMATA John Bina niseme ukweli kutoka moyoni kwangu hongereni sana kwa hatua mnayopiga,hata mimi nilivyokuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini nikiwa Bungeni nilianzisha kauli ya kuwaita wachimbaji wadogo na siyo wachimbaji wadogo wadogo maana yangu ni watu mnaokwenda hatua kwa hatua hadi kuwa wachimbaji wakubwa"amesema Mhe.Malima

Amewakumbusha FEMATA kuwa wakereketwa wa utunzaji wa Mazingira nchini hasa kutokana na uhalisia wa shughuli zao,kwani wapo baadhi yao hawazingatii hilo na badala yake wanaharibu Mazingira kuanzia kutiririsha maji yenye kemikali ambayo yana hatarisha afya za watanzania,amewahimiza Shirikisho hilo kulipa kipaumbele jambo hilo ili liwe na matokeo chanya.

"Mhe.mgeni rasmi maagizo yako yote tumeyapokea na kukuahidi kuyafanyia kazi,hii wiki ya Madini miongoni mwa mambo tunayofanya ni pamoja na kutoa elimu kwa wanachama wetu ikiwemo utunzaji wa mazingira"John Bina,Rais wa FEMATA.

"Serikali kwa kuendelea kutambua mchango wa Wachimba Madini imeweka mazingira mazuri kwao ya ufanyaji wa shughuli zao ikiwemo kuondoa changamoto zilizokuwa zinarudisha nyuma au kuchelewesha shughuli zao,ndiyo maana sasa wanazidi kupiga hatua na kuwa nguzo ya pato la Taifa" Francis Mihayo,Kamishna wa Madini.

Shirikisho la Wachimba Madini nchini kwa mara ya kwanza linafanya Mkutano wao Mkuu na wiki ya Madini Mkoani Mwanza inayokwenda pamoja na kongamano lenye lengo la kuelimishana na kuzijadili  changamoto mbalimbali zinazowakabili na kushauriana namna ya kuzitatua na pia kutoa

 ushauri na maoni yao Serikalini kuhusu kuyaboresha mazingira yao ya kazi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti