• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC Malima awapa somo wachezaji wa Pamba namna ya kupanda Ligi kuu msimu ujao

Posted on: November 2nd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amewataka wachezaji wa timu ya soka ya Pamba inayoshiriki ligi ya Championship kucheza kwa malengo na hatimaye kupanda ligi kuu msimu ujao.

Akizungumza leo na wachezaji na uongozi wa klabu hiyo kwenye uwanja mkongwe wa Nyamagana Mkuu huyo wa Mkoa amesema mchezaji anayecheza bila ya malengo huyo hafai na aondolewe kwenye timu kwenye dirisha dogo.

"Kwangu mimi nina mambo mawili ambayo sikubaliani nayo kucheza bila malengo na migogoro mkinionesha hali hiyo najiweka kando nanyi", amesisitiza Mhe.Malima

Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ameinua soka kwenye Mikoa aliyofanya kazi ya Mara na Tanga amesema hivi sasa anaendelea kutunisha mfuko wa kuendeleza soka Mkoani Mwanza na wadau wamekuwa na imani na mwendo wa timu ya Pamba hivyo amewataka wasimuangushe kwa kufanya mambo yasiyo na tija.

Aidha, Mhe. Malima kwenye Mkutano huo na wachezaji wa Pamba amewakabidhi Shilingi Milioni moja kama motisha baada ya kufanya vizuri michezo yao miwili ya ligi Daraja la kwanza kwa kuilaza Pan African bao 1-0 kabla ya kuibugiza Trans Camp mabao 2-0.

"Jiwekeeni utaratibu wa kucheza soka la kisasa na kutanguliza nidhamu hii ndiyo siri ya nyota wengii wa soka Duniani walivyofanya pia wekeni luninga kubwa kwenye hostel yenu mtakayotumia kuona mchezo mlioshiriki na kubaini makosa au sehemu mliofanya vizuri kuongeza zaidi maarifa, kwa kufanya hivyo mtawavutia wafadhili kutokana na kuwa na timu inayofanya vizuri wakati wote," Amesema Mkuu wa Mkoa.

Awali akimkaribisha Mhe. Malima, Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano

 wa klabu hiyo Aleem Alibhai amemshukuru Mkuu huyo wa Mkoa kwa moyo wa kupigania timu hiyo na kusisitiza motisha wanayopata kutoka kwa wadau inawaongezea ari ya kufikia malengo yao ya kucheza ligi kuu.

Timu ya soka ya Pamba katika msimamo wa ligi Daraja la kwanza inashika nafasi ya 6 ikiwa na mtaji wa pointi 15 na mwishoni mwa wiki hii watashuka dimbani Nyamagana kumenyana na timu ya Ndanda kutoka Mtwara.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti