• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC Malima kuweka shamba la Pamba la mfano Sengerema

Posted on: March 2nd, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amepania kuinua zao la Pamba lenye ubora kwa kuweka shamba la mfano kata ya Buyagu Wilayani Sengerema.

Akizungumza na baadhi ya wakulima alipotembelea mashamba yao ya Pamba, Mhe. Malima amesema bado wakulima wa zao hilo hawatumii kilimo cha kisasa, sasa ameamua kuwasilisha mpango wa kuweka kilimo cha kisasa Bodi ya Taifa ya Pamba baada ya kupata hekari za kutosha kwa kuwatumia wakulima ambao watakuwa tayari kuingia katika mpango huo.

"Mimi ni Mwenyekiti wa kamati ndogo ya Uzalishaji wa zao la Pamba kwenye bodi ya Taifa, nitatumia fursa ya kikao chetu kijacho huko Mkoani Simiyu kuuzungumzia mpango huu lengo ni miaka michache ijayo mkulima avune tani milioni moja." Malima amesisitiza.

Amebainisha kuwa mpango huo utahusisha kuwaleta wakulima Wataalamu watakaopima udongo, kutoa ushauri aina ya mbolea husika na namna ya upandaji kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo ili mkulima kila hekari moja apate kilo 2000.

Ameongeza kuwa mara baada ya kuyakagua mashamba hayo amesikitishwa kutokana na kuwaona wakulima wakipoteza fursa ya kupata fedha nyingi kama wangetumia ulimaji wa kisasa unaohimizwa.

"Hapa nimelima kwa kutumia utaratibu wa kienyeji tu sijatumia utaalamu wowote wala kuweka mbolea, hii imetokana na kutofikiwa na Wataalamu nikaamua nilime tu nilivyozoea." Maneno Maneno, Mkulima wa Pamba.

Mkoa wa Mwanza unalima Pamba Wilaya 4 za Sengerema,Kwimba,Misungwi, na Magu na mwaka jana imevuna Pamba kilo milioni 16.

Aidha Mhe. Malima akiwa njiani kwenda Mgodi wa Nyanzaga kupata taarifa za maendeleo ya fidia za wakazi jirani na eneo hilo, amesimama kata ya Igarula katika mkutano wa hadhara na wananchi na kuwahakikishia mradi wa maji wa Shs Bilioni 13.7 unaotekelezwa na SEWASA kuwa utakamilika kwa wakati.

Kuhusu changamoto ya uchache wa Bweni Shule ya Sekondari ya Ngoma, Mhe.Malima ameahidi kuongeza mabweni mawili la wasichana na wavulana ili kuwapunguzia adha ya kutembea umbali mrefu wanafunzi hao.

"Niwasihi sana wananchi muwe na utulivu na msikubali kudanganywa na wachache watakaokuja kwa nia ya kuchochea migogoro wakati mkiwa mbioni kulipwa fidia na Mgodi wa Nyanzaga". Amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti