• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AAGIZA KUFUNGWA MFUMO WA KUKUSANYA MAPATO ILI KUDHIBITI UPOTEVU FEDHA BUDUSHI HC

Posted on: September 14th, 2024

RC MTANDA AAGIZA KUFUNGWA MFUMO WA KUKUSANYA MAPATO ILI KUDHIBITI UPOTEVU FEDHA BUDUSHI HC


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemuagiza Katibu Tawala Mkoa kushirikiana na Mganga Mkuu wa Mkoa kuhakikisha ndani ya siku 14 wanaweka mfumo wa makusanyo na matumizi ya fedha kwenye Kituo cha Afya Budushi kilichopo kata ya Sumve wilayani Kwimba.

Ametoa agizo hilo mapema leo Septemba 14, 2024 wakati akifanya ukaguzi wa huduma za afya kwenye kituo hicho na kubaini kuwapo kwa mfumo wa makusanyo na matumzi wa makaratasi badala ya Mfumo wa kisasa wenye ufanisi na unaodhibiti upotevu wa mapato (GOTHoMIS).

Sambamba na hilo, Mhe. Mtanda amemtaka katibu tawala kwa kushirikiana na OR -TAMISEMI kuandaa mafunzo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri, Waganga Wakuu wa Wilaya na maafisa TEHAMA ili kuwajengea uwezo wa namna ya kutumia mfumo huo kwa tija na akaahidi kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo.

Aidha, ametoa rai kwa Mganga mkuu wa wilaya hiyo kuwa mbunifu na mwenye maamuzi ya haraka katika kufunga mifumo na vifaa tiba na visaidizi kwenye vutuo vya kutolea huduma ili malengo ya serikali ya kuboresha huduma za afya yaonekane mapema.

Akikagua ujenzi hususani kwenye jengo la Mama na Mtoto na kichomea taka ameagiza kasi ya ujenzi iongezwe ili hadi kufikia septemba 30, 2024 wakamilishe na huduma kwa wananchi zaidi ya elfu 17 ziendelee kutolewa katika hali ya ubora na kuwapunguzia msongamano kwenye hospitali ya Kanisa waliyokua wanapata huduma siku za nyuma.

Awali, akiwasilisha taarifa Mganga mfawidhi wa Kituo hicho Paul Kanga amesema mradi wa ujenzi wa kituo hicho umepokea kiasi cha Tshs. 656.4 milioni ambapo Tshs. 300 Milioni kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri na Tshs. 356.4 kutoka TASAF ambayo inahusisha na Tshs. 16.5 Milioni za nguvu za wananchi ambao wamenunua pia eneo kwa Tshs. 8 milioni.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti