• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AAGIZA UCHUNGUZI KUBAINI CHANZO CHA MOTO KITUO CHA AFYA KAKOBE

Posted on: September 2nd, 2024

RC MTANDA AAGIZA UCHUNGUZI KUBAINI CHANZO CHA MOTO KITUO CHA AFYA KAKOBE


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa muda wa siku kumi na nne kwa Katibu Tawala Mkoa huo Bwana Elikana Balandya kuunda timu maalumu ya kuchunguza chanzo cha tukio la moto lililotokea usiku wa kuamkia September 02 katika kituo cha afya Kakobe kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo leo Septemba 02, mara baada ya kutembelea kituo hicho  na kujionea madhara yaliyotokana na moto huo, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wananchi hao kuwa na subira katika kipindi hiki ambapo Serikali inaendelea kutafuta namna mbadala ya kuwapatia wananchi hao huduma muhimu ya matibabu.

Akiwatoa hofu wananchi zaidi ya elfu 20 wanaotumia kituo hicho, RC Mtanda amesema huduma zitaendelea kutolewa kama kawaida kwani Mganga Mkuu wa Mkoa atahakikisha anachukua hatua za dharula ili kuhamishia huduma za maabara kwenye jengo linalofaa.

Aidha, amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa kufanya tathmini kwenye uharibifu wa majengo hayo na kushauri kama yanastahili kukarabatiwa au vinginevyo ili hatua zichukuliwe mara moja za kuhakikisha huduma zinarejeshwa kwenye kata hiyo ya Kazunzu.

Akitoa taarifa ya tukio hilo la moto, Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dkt. Vita Ndohele amesema chanzo cha moto huo inasemekana ni hitilafu ya umeme katika chumba cha maabara na kupelekea kuungua kwa jengo la wagonjwa wa nje ambalo lina vyumba saba, kuteketea kwa vifaa tiba pamoja na dawa vilivyokua vikitumika ndani ya vyumba hivyo huku hasara ya dawa na vifaa tiba ikisemekana kuwa ni zaidi ya thamani ya shilingi Milioni 100.

Halikadhalika, amewashukuru wananchi kwa utulivu na ushirikiano katika kuokoa vitu visiteketee mara tu baada ya madhira hayo kutokea majira ya saa 7 usiku wa kuamkia leo kabla ya Taasisi ya uokoaji ya zimamoto kuwasili kwa msaada zaidi kutokana na umbali uliopo kutoka Mkoani.

Kituo hicho kilichoanzishwa tangu mwaka 1986 kimekua tegemeo kwa zaidi ya wananchi elfu 20 kutoka kwenye tarafa nzima ya Kakobe.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti