• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AFUNGA RASMI MICHEZO YA SHIMISHEMITA MWANZA

Posted on: September 5th, 2024

RC MTANDA AFUNGA RASMI MICHEZO YA SHIMISHEMITA MWANZA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda akimuwakilisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) leo Septemba 5, 2024 amefunga rasmi Michezo ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa (SHIMISEMITA) kwenye uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza.

Akizungumza na wanamichezo hao Mhe. Mtanda amesema Serikali ya awamu ya sita imedhamiria kuinua sekta ya michezo, sanaa na utamaduni na ni muhimu kwa watumishi wa Serikali kumuunga mkono mchezaji namba moja nchini ambaye ni Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kushiriki katika michezo hiyo iliyoandaliwa kwa ajili yao.

"Michezo mahala pa kazi inawajengea ari ya kuchapa kazi kwani ukamilifu wa afya inawajengea uwezo mkubwa wa kufanya kazi tena kwa weledi, huku mkiwaa mmeimarika wakati wote lakini pia ina wajengea uzalendo." RC Mtanda.

Aidha, amewataka wanamichezo hao kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za michezo ili malengo ya shirikisho hilo yatimie na ametumia jukwaa hilo kuzionya Halmashauri zilizokiuka taratibu na kupelekea kuondolewa kwenye michezo hiyo kuhakikisha hawafanyi hivyo tena kwani kuwapelekea watumishi kuwakosesha haki yao ya kujumuika na wenzao katika michezo.

Sambamba na hayo Mhe. Mtanda piaa amewapongeza wanamichezo kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela na Wilaya ya Kwimba kwa Mkoa wa Mwanza kwa kushika nafasi za tatu kwenye baadhi ya michezo.

Awali, Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo Henry Kapela alibainisha kuwa jumla ya wanamichezo 2160 kutoka kwenye Halmashauri 100 wameshiriki mwaka huu tofauti na 45 za mwaka jana na kwamba uhamasishaji na maandalizi ya michezo ya mwakani unapaswa kuanza sasa.

Vilevile, ametoa rai kwa uongozi wa mashirikisho hayo ngazi ya Halmashauri kuzingatia taratibu na sheria za michezo chini ya shirikisho hilo ili kuwaepusha na usumbufu wa kuondolewa kama ilivyotokea kwa halmashauri 3 ambazo ni Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Dodoma na Manispaa ya Moshi.

Mshindi wa jumla wa michezo ya SHIMISEMITA kwa mwaka huu ni Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambao wamekua wa kwanza kwa michezo 9. Aidha  michezo hiyo kwa mwaka huu imechagizwa na kaulimbiu isemayo "Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Taifa Endelevu".

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti