• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AHIMIZA ULIPAJI KODI, UWAJIBIKAJI NA AMANI

Posted on: December 24th, 2024

RC MTANDA AHIMIZA ULIPAJI KODI, UWAJIBIKAJI NA AMANI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda amewataka viongozi wa Chama na Serikali kuhimiza na kusimamia ulipaji kodi kwa maendeleo ya Taifa.

Ametoa agizo hilo leo Disemba 24, 2024 wakati akihitimisha kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa huku akisisitiza kuwa ili serikali iweze kutoa huduma bora kwa wananchi na kuwaletea maendeleo ni lazima iwe na fedha.

"Machafuko tunayo yashuhudia hivi sasa ulimwenguni baadhi yanatokana na hasira za wananchi kukosa huduma za msingi huku Serikali ikikosa fedha kutokana na kushindwa kukusanya kodi", Mhe. Mtanda.

Aidha, amewaomba viongozi kushirikiana kuhakikisha nidhamu ya ulipaji kodi inakuwepo na Serikali kuendelea na mkakati ya kuwaletea maendeleo wananchi wake.

Akizungumza kuhusu uwajibikaji Mkuu huyo wa Mkoa amewataka watumishi kuweka mbele nidhamu ya uwajibikaji kwa wananchi na kuepukana na vitendo vya rushwa.

"Viongozi wote mliopo hapa mkiwemo wakuu wa Wilaya na Taasisi kasimamieni hili msimuonee mtu aibu kumchukulia hatua, wananchi wana Imani na Serikali hii ya kuwapa huduma bora",amesisitiza Mtanda wakati wa kuhitimisha kikao hicho.


Hali kadhalika, amehimiza amani na hasa katika kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka kwa kuwataka wananchi kuwa watulivu na kuepukana na aina yoyote ya uvunjivu wa amani huku dola likiwa makini wakati wote kuhakikisha usalama wa wananchi na mali zao.

Katibu Tawala Mkoa wa

Mwanza Ndg. Balandya Elikana akijibu hoja ya mbunge wa Ilemela Mhe. Anjelina Mabula kuhusu ulipwaji wa fidia kaya 300,000 waliopisha maeneo yao kwa ajili ya upanuzi wa uwanja wa ndege, amesema mchakato wote umekamilika kinachosubiriwa ni mrejesho kutoka mamlaka husika.

Kikao hicho cha Kamati ya Ushauri Mkoa kimepokea hoja ya Jimbo la Magu kugawanywa sehemu mbili na kuwepo Jimbo lingine la Sanjo kutokana na ukubwa na idadi ya wananchi zaidi ya laki nne huku hoja ya Jimbo la Sengerema kugawanywa na kuwepo na Jimbo la Karumo likitolewa maelekezo ya kufanyika kikao cha kitaalamu kabla ya kuwasilishwa kikao kijacho cha RCC.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti