• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO NA KUFUNDISHIA VYENYE THAMANI YA ZAIDI YA MILIONI 36 MISUNGWI

Posted on: February 12th, 2025

RC MTANDA AKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO NA KUFUNDISHIA VYENYE THAMANI YA ZAIDI YA MILIONI 36 MISUNGWI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo tarehe 12 Februari, 2025 amekabidhi vifaa vya kufundishia na michezo vyenye thamani ya zaidi ya Tshs. Milioni 36 kwa shule 3 za Sekondari Wilayani Misungwi vilivyototelewa na Taasisi ya Africa School House.

Akiongea mara baada ya kukabidhi msaada huo katika hafla iliyofanyika katika shule ya sekondari ya Aimee Milembe, Mhe. Mtanda amewashukuru wahisani hao kwa msaada huo muhimu kwa maendeleo ya sekta ya elimu Wilayani humo na Mkoa wa Mwanza kwa ujumla.

"Elimu ndio mtaji mkubwa katika maisha na tunaamini kwenye kuwekeza kwa watoto na katika kufanikisha hilo Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan inatoa fedha nyingi kwenye elimu na tunawashukuru washirika wetu kwa kuwa nasi tangu mwaka 2017 kwa kujenga shule sehemu mbalimbali, nyumba za walimu, visima virefu vha maji." RC Mtanda.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amesema ndani ya miaka minne shule mpya 11 za sekondari zimejengwa, mabweni 30, nyumba 12, matundu vya vyoo 133 kwa sekondari na kwamba awali zilikuwepo shule 965 za msingi na sasa 1043 sawa na ongezeko la shule 85 na shule 275 hadi 332 za sekondari sawa na ongezeko la shule 57.

Mhe. Mtanda ameongeza kuwa ndani ya kipindi cha miaka 4 walimu 1168 wameajiriwa na kupangiwa vituo ndani ya Mkoa huo na kwamba Serikali imepata mafanikio kwa kuwa na miundombinu hivyo basi wahisani hao kuunga mkono juhudi hizo ni jambo la msingi sana.


Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Dkt. Aimee Bessire amesema wanayo furaha kusaidia sekta ya Elimu na siyo tu kwa vifaa hivyo bali wanajenga pia miundombinu kama mabweni, madarasa, vyoo na jiko wilayani humo vinavyogharimu zaidi ya Tshs. milioni 350.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti