• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AKUTANA NA WATUMISHI NA KUHIMIZA UBUNIFU, UWAJIBIKAJI NA KUWAJALI WANANCHI

Posted on: April 9th, 2024

RC MTANDA AKUTANA NA WATUMISHI NA KUHIMIZA UBUNIFU, UWAJIBIKAJI NA KUWAJALI WANANCHI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo  amekutana na watumishi wa Ofisi ya mkuu wa Mkoa, Wakurugenzi na Wakuu wa idara kutoka halmashauri zote nane na kusisitiza uwajibikaji wenye weledi, ubunifu kwenye ukusanyaji Mapato, Usimamizi wa Miradi na kusikiliza kero za wananchi.

Akizungumza na watumishi hao kwenye kikao kazi hicho kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa Mkoa, Mhe.Mtanda aliyetumia nafasi hiyo pia kujitambulisha ameweka bayana anataka kuona Halmashauri zikiongeza ubunifu wa vyanzo vya mapato ili Serikali iweze kuweka mipango imara ya maendeleo.

"Ndugu watumishi wenzangu tuna wajibu wa kutimiza ndoto za Rais Samia za kuona kasi ya maendeleo kwa wananchi, tukasimamie miradi na ikamilike kwa wakati," Mkuu wa mkoa.

Mkuu huyo wa mkoa aliyehamishiwa hivi karibuni kituo cha kazi Mwanza akitokea Mara,amesema yupo mbioni kuanza ziara wilayani akianzia Ukerewe lengo ni kusikia kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.

Aidha amemshukuru Rais Samia kwa kuendelea kumuamini na kuahidi kufanya kazi kwa uaminifu,uadilifu na kuwatendea mema wananchi.

Ameongeza siku chache zilizopita amekutana na viongozi wa dini,wakuu wa wilaya wakishauriana mambo kadhaa ya kiutendaji na leo anakutana na watendaji wa shughuli za Serikali ambao ni watu muhimu katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Akitoa neno la shukurani mara baada ya hotuba ya mkuu wa mkoa,Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza Bw.Balandya Elikana amesema maagizo yote yamepokelewa na kufanyiwa kazi.

"Mhe.mkuu wa mkoa nakuahidi tutakujibu kwa vitendo kwa uchapakazi bora na wenye tija kwa wananchi,hatuna shaka na uwajibikaji wako ambao utakuwa mfano kwetu sisi",Balandya.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti