• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA ALIVALIA NJUGA TATIZO LA USAFIRI ENEO LA KIVUKO CHA KIGONGO-BUSISI

Posted on: February 2nd, 2025

RC MTANDA ALIVALIA NJUGA TATIZO LA USAFIRI ENEO LA KIVUKO CHA KIGONGO-BUSISI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amelazimika kuamuru mabasi na magari madogo kupita kwenye daraja la muda la mkandarasi eneo la Kigongo Busisi kutokana na kivuko cha MV Sengerema kuharibika injini na kusababisha hali ya uvukaji kuwa mgumu.

Akizungumza na wananchi eneo la kivuko leo Februari 2, 2025 wananchi waliokaa muda mrefu kusubiri kuvuka kuelekea Sengerema na mikoa ya Geita, Kigoma Kagera, Mtanda amesema tatizo hilo limesababishwa na hali mbaya ya magugu maji yaliyotapakaa ziwani humo na kusababisha uharibifu wa injini ya Mv Sengerema.

Amesema tayari amechukua hatua mbili,mosi amefanya mawasiliano na Wizara husika na masuala ya mazingira ili kuwaleta wataalam na wadau wengine wanaopambana na mazingira  kuja kufanya utafiti wa kuyaondoa magugu maji hayo na pili amezungumza na Waziri wa Ujenzi ili alete injini mojawapo inayotarajiwa kufungwa kwenye vivuko vipya vitano vinavyojengwa hapa Mwanza.

"Poleni kwa usumbufu ndugu zangu wananchi tuwe na subira kidogo hali itatengemaa,tayari hatua za msingi nimefanya," amesisitiza mkuu huyo wa mkoa wakati anazungumza na wananchi hao.

Mtanda ambaye amelazimika kusimamia pande zote mbili Kigongo na Busisi upitaji wa magari hayo kwenye daraja la muda la mkandarasi,wasafiri hao walionesha furaha na kumshukuru mkuu huyo wa mkoa kwa kuwakwamua baada ya kusota kwa saa nyingi kusubiri kuvuka.

"Nimekaa hapa kuanzia saa 8 mchana na sikuwa na matumaini ya kuvuka mapema na safari yangu ni Geita,tunamshukuru sana mkuu wa mkoa kwa kutupatia ofumbuzi," Richard Mahizo,msafiri

Kivuko cha Mv Sengerema kimesimama kutoa huduma hii ni wiki ya pili kutokana na injini yake kuharibika na kusalia vivuko viwili vinavyotoa huduma hata hivyo vimee lol elewa kutokana na idadi kubwa ya wasafiri na magari yanayopita eneo hilo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti