• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AMEWATAKA WANANCHI KUDUMISHA AMANI NA KUFANYA KAZI KUJITAFUTIA MAENDELEO

Posted on: June 7th, 2024

RC MTANDA AMEWATAKA WANANCHI KUDUMISHA AMANI NA KUFANYA KAZI KUJITAFUTIA MAENDELEO


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wananchi kuimarisha amani na kufanya kazi kwa bidii ili kujitafutia kipato na kuweza kuinua kipato na uchumi wao.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo jioni Juni 07, 2024 kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Misasi katika kata ya Misasi wilayani Misungwi ambapo alibaini uwepo wa vijana wavivu wasioshiriki kazi za kuleta maendeleo na badala yake wanajihusisha na uhalifu.

"Nataka kuona hatua kali zikichukuliwa dhidi ya wananchi wahuni wanaoharibu amani ya watu wengine kwa kujihusisha na wizi, kucheza Pool Table, ujambazi na uvutaji wa bangi na kila aina ya uhalifu" Mtanda.

Akisisitiza kuhusu umuhimu wa kulinda amani, Mhe. Mtanda ametumia wasaa huo kuwaonya Sungusungu ambao hutumika kama askari wa jadi wanaozuia uhalifu kuacha tabia ya kuwakamata na kuwapiga wahalifu badala yake wawafikishe kwenye vyombo ya sheria.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi kuacha kuingiza mifugo kwenye shamba la Serikali la mifugo la Mabuki kwani kufanya hivyo kunaharibu juhudi za Serikali za kuinua sekta ya mifugo kwa kuwaletea shamba darasa na ameagiza kutungwa kwa sheria ndogo kali kwa ajili ya kuwaadhibu wanaolisha mazao.

Mwalimu Diana Kuboja, Afisa Elimu wa Sekondari amewapongeza wananchi wa Mwasagera kwa kujenga shule ya sekondari kwa nguvu zao kwa asilimia 100 na imesajiliwa na kwamba ifikapo Julai 01, 2024 watoto wataanza kusoma kwani itafunguliwa.

Dkt. Clement Morabu, Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo amesema kuwa kutokana na uchakavu wa kituo cha Afya wamepeleka ombi maalum la kufanyiwa ukarabati na upanuzi wa kituo hicho na kwamba kwa sasa wamejengewa Jengo la Mionzi kutokana na fedha kiasi walizozipata.

Awali, Diwani wa Kata ya Misasi Mhe. Daniel Busalo amenainisha kuwa ndani ya kata hiyo wameshapokea fedha zaidi ya Bilioni moja kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo na zaidi ya milioni 194 kutokana na fedha za ushuru yaani mapato ya ndani ya halmashauri hiyo.

Awali, Bi. Veronica Heneriko mkazi wa kijiji cha Misasi ameelezea kero ya mmomonyoko wa maadili kwa vijana ambapo amebainisha kuwa wanatumia dawa za kulevya hususani bangi na kwamba wanateseka na adha ya maji na kwamba ni kijiji cha Manawa pekee ndio wanaopata maji.

Martine Mashamba kutoka kijiji cha Mwasagera ameelezea changamoto ya watoto kufuata elimu ya Sekondari kwa umbali mrefu kutokana na kijiji hicho kukosa Shule ya Sekondari na kulazimika watoto kutembea hadi kijiji jirani na kusababisha utoro.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti