• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA APIGA GIA ANGANI ATANGAZA MOTISHA PAMBA JIJI IKISHIKA NAFASI ZA JUU LIGI KUU

Posted on: February 15th, 2025

RC MTANDA APIGA GIA ANGANI ATANGAZA MOTISHA PAMBA JIJI IKISHIKA NAFASI ZA JUU LIGI KUU


Timu ya soka ya Pamba Jiji FC ambayo mzunguko wa lala salama ya ligi kuu imeingia na gia kubwa kwa kutoa dozi za ushindi kwa timu pinzani, sasa imetangaziwa dau nono endapo itamaliza ligi hiyo huku ikiwa imeshika nafasi za juu kuanzia ya tano hadi kumi.

Akizungumza na wachezaji wa Pamba Jiji mapema leo Ofisini kwake kabla ya timu hiyo kushuka dimbani kumenyana na Wagosi wa Kaya (Coastal Union), Mtanda amesema awali malengo yalikuwa msimu huu ni kuhakikisha wanabaki ligi kuu.


Ameongea kuwa, kutokana na mwendo mzuri walionao malengo ni kushika nafasi za juu na hilo linawezekana endapo watashinda mchezo dhidi ya Coastal Union na Mashujaa FC.

"Mkakati wa kupigania kubaki ligi kuu huo sasa tunaugeuzia kisogo, tuanze kupigania nafasi za juu na motisha nono itakuwepo tukishika nafasi ya tano au kumi,"amesisitiza Mtanda ambaye pia ni mlezi wa Pamba Jiji.


Amewakumbusha wachezaji hao kuongeza bidii kwa kila mchezo wao kwani lala salama ya ligi kuu ni ngumu na waepuke aina yoyote ya utovu wa nidhamu ambao utaigharimu timu.

"Epukeni kufanya madhambi dimbani na kupewa umeme (akimaanisha kadi nyukendu) hii itasabisha mzigo kwa timu kwa kumkosa mchezaji muhimu." Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Katika mazungumzo hayo Mtanda amewakabudhi wachezaji hao Tshs. milioni 11 mchango aliopewa na wadau wa soka walioamua kumchangia na kubaki milioni 4 ili zikamilike milioni 15 ahadi aliyowapa wachezaji hao ya shs milioni 30 baada ya ushindi wao dhidi ya Azam FC,awali aliwakabidhi milioni 15.

Katika mpambano wake wa leo uliopigwa dimbani CCM Kirumba Wana TP Lindanda wamezidi kuwasha endiketa kuelekea nafasi za juu katika msimamo wa ligi kuu baada ya kuwachezesha ngoma ya Mdumange timu ya Coastal Union kutoka Tanga kwa kuwabugiza mabao 2-0.

Kwa ushindi huo timu hiyo sasa imekwaa hadi nafasi ya 8 na mtaji wa pointing 21 kibindoni huku ikijiandaa na safari ya Kigoma kuwafuata Mashujaa FC  mchezo utakaopigwa siku ya Jumatano Februari 19 kwenye uwanja wa Lake Tanganyika.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti