• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA ATOA WITO KWA TAASISI NCHINI KUTENGA FEDHA ZA WATUMISHI KUSHIRIKI MICHEZO

Posted on: September 2nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa wito kwa wakuu wa taasisi na mashirika nchini kutenga fedha za michezo na kuzitumia kwa mujibu wa vifungu vya michezo ili kuimarisha afya ya watumishi.

Ametoa maagizo hayo leo tarehe 02 Septemba, 2025 wakati akifungua mafunzo na semina kwa Viongozi, makocha na madaktari wa Michezo kutoka shirikisho la michezo ya Mashirika ya umma, taasisi na makampuni binafsi Tanzania ( SHIMMUTA).

Amesema sera za nchi zinawataka wakuu wa taasisi na mashirika kutenga fedha na kutoa kwa wakati kwa washiriki wa michezo kwenda kujumuika na wengine wakati wa kalenda ya michezo katika mikoa mbalimbali wanayokutana.

Ameongeza kuwa wafanyakazi wanaoshiriki michezo wanakua na afya thabiti hawaugui ovyo na wataleta tija kwenye ofisi kwa kupata watumishi wenye afya njema wakati wote.

Vilevile, ametoa wito kwa taasisi hizo kudhamini na kuandaa mabonanza na michuano mbalimbali ya ndani ili watumishi washiriki michezo kabla ya wakati wa kukutana kwa ajili ya michezo ya SHIMMUTA.

“Mafunzo ni sehemu ya kuboresha michezo nchini, nimeambiwa hapa wapo hadi madaktari na kweli watu wote hawa wanatakiwa kupata mafunzo ya uongozi na sio tu kutoa tiba hivyo nawapongeza maana mnawapa uwezo wa kuandaa timu kikamilifu.” Amesema Mhe. Mtanda.

Akitoa risala ya wanachama, Mwenyekiti wa SHIMMUTA Ndugu Roseline Masamu amesema mafunzo kama hayo mwaka 2023 walikua 110, 2024 walikua washiriki 114 lakini mwaka 2025 wana washiriki 130, ongezeko linaloonesha kuwa wakuu wa taasisi wanatambua umuhimu wa michezo nchini.

Aidha, amebainisha kuwa semina hiyo iliyozikutanisha taasisi 59 inakwenda sambamba na maandalizi ya michezo inayoratibiwa na umoja huo ambayo inatarajia kurindima mwezi novemba ndani ya Mkoa wa Mwanza.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti