• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWAAGIZA JIJI LA MWANZA KUMPA KAZI MKANDARASI ATAKAYEWEZA KUJENGA SOKO LA MCHAFU KUOGA USIKU NA MCHANA

Posted on: June 3rd, 2024

RC MTANDA AWAAGIZA JIJI LA MWANZA KUMPA KAZI MKANDARASI ATAKAYEWEZA KUJENGA SOKO LA MCHAFU KUOGA USIKU NA MCHANA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka Halmashauri ya jiji la Mwanza kuhakikisha wanampata Mkandarasi atakayefanya kazi usiku na mchana katika mradi wa ujenzi wa soko la wafanyabiashara wadogo la mchafukuoga ili lijengwe kwa kasi.

Amesema hayo leo Juni 03, 2024 wakati akiwa kwenye ziara ya ukaguzi wa huduma kwenye soko hilo lililopo kata ya Igogo na akabainisha kuwa ndani ya miezi sita wananchi watapata soko la kisasa lenye miundombinu ya Maji, Vyoo na nishati ya Umeme.

Amesema, ni lazima Halmashauri ihakikishe inalinda fedha zinazotolewa na Mhe. Rais kwa ajili ya ujenzi wa miradi na kwamba yeye kama msimamizi hatokubali kuona fedha za umma zikichezewa na watu wachache kwa kufanya ubadhirifu na atakayethubutu atamchulia hatua za kisheria.

Aidha, amebainisha kuwa Serikali itasaidi kuweka utaratibu wa kuwaunganisha wafanyabiashara wa Kanda ya ziwa ili kulifanya Soko hilo kuwa kitovu cha Uuzaji wa Mitumba ya nguo na kwamba hali hiyo itasaidia hata kuleta watalii kwenye soko hilo.

Hatahivyo, amezitaka Mamlaka zinazohusika na maji yaani MWAUWASA, TANESCO-Umeme, TARURA kwa ajili ya barabara pamoja na Halmashauri kuboresha huduma zote zinazowahusu  ili wafanyabiashara hao wapate ridhiki kwenye eneo linalofaa na wasihatarishe afya zao.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Nyamagana alibainisha historia ya uwepo wa wafanyabishara hao kuwa ni kutokana na kupangwa kutoka uuzaji holela waliokua wakishiriki siku za nyuma kwa kuuza nguo mjini kwenye hifadhi ya barabara.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Mwanza Peter Lehhete amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa siku za karibuni atapatikana Mkandarasi wa ujenzi wa Soko hilo kwani tayari Halmashauri ipo kwenye taratibu za manunuzi na kwamba wametenga shilingi Bilioni 7 kujenga soko la Kisasa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti