• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWAPONGEZA H/ ILEMELA KWA KUOKOA MIL. 26 UJENZI WA MADARASA

Posted on: July 12th, 2024

RC MTANDA AWAPONGEZA H/ ILEMELA KWA KUOKOA MIL. 26 UJENZI WA MADARASA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kwa kuokoa fedha takribani Milioni 26 zilizobakia katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa vyumba 44 vya madarasa Idara ya elimu msingi.

Pongezi hizo amezitoa mapema leo Julai 12, 2014 alipokua katika hafla fupi ya kukabidhiwa vyumba 44 vya madarasa Wilayani Ilemela, hafla iliyofanyika katika shule ya Sekondari ya Lumala iliyopo Kata ya Ilemela, Manispaa ya Ilemela kwa kumkabidhi Mkuu huyo wa Mkoa vyumba 06 vya madarasa kuwakilisha vingine.

"Ninawapongeza kwa kuokoa fedha takribani Milioni 26, na ni msimamamo wa Serikali kwamba tunapofanya shughuli za ujenzi wa miradi ya maendeleo siyo lazima fedha zote zitumike, tunaweza kuokoa fedha na tukazitumia kwa shughuli nyingine".Mtanda

Maeneo mengine wangeweza kula fedha hizo, na madarasa haya 44 yasingekamilika na sasa tungekua tunapelekana TAKUKURU huko, kwa hiyo ninawapongeza sana kwa kuokoa fedha hizo. Amesema Mkuu huyo wa Mkoa.

Aidha, Mhe. Mtanda pia ametoa rai kwa wanafunzi hao kuendelea kujiimarisha kwa kusoma kwa bidii, juhudi na maarifa kwa kuwa Serikali ya Rais Samia imedhamiria kufanya mageuzi makubwa katika sekta ya elimu kwa kuboresha miundombinu kadhalika kuwatimizia maslahi ya walimu.

"Siku hizi kuna msemo unasema kwamba elimu ya zamani ni tofauti na ya sasa, ndio ni kweli ukitizama hata madarasa haya yanavutia yana vigae, madirisha mazuri, umeme kwa ajili ya mwanga, sasa na nyie wanafunzi someni kwa bidii",amesisitiza mkuu huyo wa mkoa.

Sambamba na hayo, Mkuu wa Mkoa pia amewataka wazazi kuweka utaratibu wa kuwa karibu na watoto wao, kwa kuwa siku za hivi karibuni kumekuwa na mmonyoko wa maadili kwa watoto hivyo amewataka kusaidia katika malezi kwa kuweka utaratibu wa kuwachunguza watoto mara baada ya kutoka shuleni.


"Unakuta mzazi ametingwa kutafuta maisha wanawatekeleza watoto kwa kuwaacha wajilee wenyewe, halafu mwisho wa siku wanakuja kushtuka wanakuta tayari watoto wameshaharibika na hizo fedha zenyewe hujapata kwa hiyo kuweni makini". Mkuu wa Mkoa akisisitiza malezi bora.


Naye, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe. Hassan Masalla amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ilipokea jumla ya shilingi 1,417,100,000,000.00 kati ya shilingi 2,261,000,000.00 iliidhinishwa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya elimu ya Sekondari, aidha kiasi cha Tshs. 1, 100,000,000.00 ni kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 44 vya madarasa, shilingi 187,500,000.00 ni ukamilishaji wa maboma 15 ya vyumba vya madarasa na seti ya meza na viti 2,750.


"Utekelezaji wa miradi hiyo umekamilika kwa 100% ambapo fedha iliyotumika ni 1,394,453,977.22 na bakaa ni shilingi 26,646,022.78". Amesema Mhe. Masalla.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti