• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWATAKA AFD KUTOA BARUA YA KUTOKUWEPO NA KIPINGAMIZI KATIKA MIRADI INAYOENDELEA

Posted on: June 4th, 2024

RC MTANDA AWATAKA AFD KUTOA BARUA YA KUTOKUWEPO NA KIPINGAMIZI KATIKA MIRADI INAYOENDELEA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Juni 04, 2024 ofisini kwake amekutana na kufanya kikao kifupi na Mkurugenzi wa Afrika Mashariki wa Shirika la Maendeleo la ufaransa (AFD Agence Francaise de Developpment) Bibi Hellen Ngarmin ambaye yupo Jijini Mwanza kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na MWAUWASA na iliyopangwa kutekelezwa.

Akizungumza katika kikao hicho RC Mtanda ametoa rai kwa AFD kutoa barua ya kuondoa vipingamizi katika mradi wa ujenzi ili kuruhusu kuendelea na hatua inayofuata kwenye mchakato wa ujenzi wa mradi wa usambazaji mabomba na ujenzi wa matenki katika upanuzi wa mradi wa maji Butimba.

Aidha Mhe. Mtanda amesema Serikali na Wananchi wa Mwanza wanatamani kuona huduma ya usambaji maji inatekelezwa katika maeneo husika na kukamilika kwa wakati ili jamii iondokane na adha ya upungufu wa maji hivyo ni wakati sasa wa kuongeza kasi kwenye taratibu za utekelezaji.

"Mradi wa Butimba ni muhimu sana kwa kuwa hapo kabla tulikuwa na mradi tegemezi wa chanzo cha kapripoint ambao haukuwa unatosheleza mahitaji hivyo kukamilika kwa mradi huu utawanufaisha watu wengi". Amesema RC Mtanda.

Mhe. Mtanda amesema pia Mwanza ni Mkoa wa Pili kwa ukubwa na ni mji wa kiuchumi hivyo uboreshaji wa sekta ya maji utapelekea watu wengi kuvutika na kufanya uwekezaji na makazi hali ambayo itapelekea uchumi wa Mwanza kukua na kuongeza muingiliano wa watu kutoka Afrika Mashariki ambao wameunganishwa na ziwa Viktoria.

Sambamba na ufadhili wa mradi wa maji wa Butimba RC Mtanda amewashukuru AFD kwa kuendelea kufadhili miradi mingine ya kimkakati kama vile ujenzi wa matundu 104 ya vyoo kwa shule za msingi, masoko na Zahanati katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela.

Naye Mkurugenzi wa Afrika Mashariki wa Shirika la Maendeleo la ufaransa (AFD Agence Francaise de Developpment) Bibi Hellen Ngarmin amesema anefurahishwa na kasi ya maendeleo ya usambaji wa huduma ya maji hasa kwa wakazi wanaoishi katika milima.

Viongozi hao kutoka Shirika la Maendeleo la ufaransa (AFD Agence Francaise de Developpment) Wametembelea Soko la  Mwaloni pamoja na miradi ya maji taka na mradi wa upanuzi wa chanzo cha Maji Safi Butimba awamu ya pili (Phase II)

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti