• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWATAKA RUWASA KUFIKISHA MAJI MWASONGWE - MISUNGWI

Posted on: September 13th, 2024

RC MTANDA AWATAKA RUWASA KUFIKISHA MAJI MWASONGWE - MISUNGWI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Misungwi kuhakikisha wanafikisha Maji kwenye kijiji cha Mwasonge kupitia mpango wa upanuzi wa mradi wa Maji wa Kigongo- Busisi wenye thamani ya zaidi ya Bilioni 6.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo leo tarehe 13 Septemba, 2024 wakati akizungumza na wananchi wa kijiji hicho katika ziara yake aliyoifanya mahsusi kwa ajili ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi na kuibuliwa kero hiyo dhidi ya RUWASA.

Mhe. Mtanda amesema RUWASA ina wajibu wa kutumia ubunifu kuhakikisha wananchi wanafikishiwa maji kwa kutumia miradi mikubwa inayotekelezwa sehemu mbalimbali kwa kutumia chanzo cha maji ya ziwa victoria na akawataka ndani ya siku 4 kuhakikisha wanatoa elimu kupitia mkutano wa kijiji kuhusu lini wanawafikishia huduma hiyo.

Naye, Kaimu Meneja wa RUWASA Misungwi Mhandisi Richard Mlilwa amebainisha kuwa mapema mwaka 2025 wananchi wa Mwasonge watafikishia Maji  kupitia Mradi huo ambapo tayari usanifu umeshafanyika na kupata mtandao wa kilomita 25 na kwamba wataweka vituo 12 vya kuchotea Maji na tanki lenye ujazo wa Lita 650,000.

Aidha kufuatia kero ya ndugu Issa Omary aliyoiwasilisha katika mkutano huo inayohusiana na masuala ya usalama, Mkuu wa Mkoa ameliagiza jeshi kuhakikisha ndani ya siku 7 wanawakamata wahalifu waliovunja maduka 5 na kuiba mali kwenye kijiji hicho usiku wa kuamkia Septemba 13, 2024 na wafikishwe mahakamani.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti