• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWATAKA SENGEREMA DC KWENDA KUJIFUNZA TARIME DC UENDESHAJI MIRADI YA CSR

Posted on: November 25th, 2024

RC MTANDA AWATAKA SENGEREMA DC KWENDA KUJIFUNZA TARIME DC UENDESHAJI MIRADI YA CSR


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kwenda kutembelea na kujifunza Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Mkoani Mara kuhusu upokeaji na uendeshaji wa fedha za Uwajibikaji wa Kampuni kwa Jamii (CSR) zinazotolewa na Migodi ya Dhahabu ili kuleta ufanisi na manufaa kwa wananchi wanaozunguka mgodi wa Sotta.

Mkuu wa Mkoa ametoa wito huo mchana wa leo   Novemba 25,2024 wakati wa hafla ya kukabidhi Madawati 1131 na samani mbalimbali zenye thamani ya jumla ya Tshs. Milioni 93.8 vilivyotolewa na Mgodi wa Sotta mining Co. Ltd uliopo Wilayani Sengerema.

Akizungumza na wananchi baada ya makabidhiano hayo Mhe. Mtanda amewashukuru viongozi wa mgodi huo kwa kuwa sehemu ya jitihada za Serikali za kuwaondoa watoto kwenye adha ya kusongamana na kukaa chini kwa kuwapatia samani hizo.

Aidha, ameitaka Halmashauri hiyo kutoa elimu kwa vijiji ili wajiandae na kuunda kamati za Uwajibikaji wa Fedha za Kampuni kwa jamii (CSR) ili uzalishaji utapoanza waweze kukidhi kanuni zilizopitishwa na tume pamoja na wizara ya Madini.

"Na niwashauri tu muende mkajifunze kule Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Musoma na Butiama wao wameanza zamani wana uelewa wa kutosha kuhusu CSR na mimi nilikuwa huko kwa hiyo ninaelewa".

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Ndugu Binuru Shekidele amewashukuru na kusema mgodi umewapunguzia adha na kwamba kwa msaada huo watabaki na upungufu wa madawati elfu 12 tu kwa shule za msingi.

Kwa upande wake Afisa Mahusiano kutoka Kampuni ya Mgodi wa Sota Bi. Habiba Said Amesema madawati na samani hizo zimetolewa ikiwa na lengo la kuimarisha mahusiano kwa kuwa bado mgodi huo haujaanza kufanya kazi na wanatarajia kuanza kutoa CSR pindi mgodi huo utakapoanza uzalishaji.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti