• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWATAKA VIONGOZI WA DINI KUISAIDIA SERIKALI KUJENGA MAADILI MEMA

Posted on: February 20th, 2025

RC MTANDA AWATAKA VIONGOZI WA DINI KUISAIDIA SERIKALI KUJENGA MAADILI MEMA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka Viongozi wa Dini kulitumia kundi kubwa la Waumini wanaowategemea kuwapelekea habari njema za kiroho ili wawe na utamaduni wa kuwa na matendo mema kwa kutumia imani zao.

Mkuu wa Mkoa ametoa rai hiyo mapema leo tarehe 19 Februari 2025 alipokuwa akitoa salamu katika Mkutano wa Sinodi Kuu (Baraza Kuu la Kanisa la Africa Inland Church Buzuruga Mwanza), ambapo amewataka Viongozi hao kuwakumbusha waumini wao wajibu wa kuishi maisha yenye maadili mema.

“Tukishirikiana vizuri kati ya Serikali na Viongozi wa Dini tutajenga Taifa lenye Watu Waadilifu na hivyo kupunguza kero nyingi zinazoikabili jamii katika

Nchi yetu”. Mhe. Mtanda.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amesema uhusiano kati ya Serikali na Dini ni vitu ambavyo havitenganishiki, ni sura mbili za sarafu. Kwa sababu, binadamu ni

mwili na roho na kila kimoja hakina budi kuendelezwa kwani Serikali inashughulika na miili na akili huku Dini zinashughulika na roho.

“Naomba niwahakikishie AICT pamoja na ndugu zetu wanaounga mkono kazi mnazofanya kwamba serikali itaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwenu ili muweze kutimiza malengo yenu ya kulijenga Kanisa na kuwahudumia Watanzania”.

Kabla ya kuhitimisha hotuba yake Mkuu wa Mkoa amesisitiza kuhusu masula mbalimbali ikiwemo Umoja na mshikamano, kukuza Amani na Utulivu, kuongoza kwa hekima na uwajibikaji, huku akiwataka Viongozi hao wakizingatia maslahi ya jamii yote na kuwahudumia waumini kwa uaminifu na upendo.

Akizungumza Kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa, Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT Mhashamu Baba Askofu Musa Masanja Magwesela, amesema Sinodi Kuu iliyoketi leo inaundwa na Dayosisi 7 yani Dayosiis ya Geita, Mara ukerewe, shinyanga, Tabora, Pwani, na Tanga ambapo wachungaji wote wa Makanisa, Viongozi wa idara, wanawake na vijana wanakutana mara moja kwa miaka miwili ambapo kwa mara ya mwisho  waliketi mwaka 2022.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti