• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWATAKA WAFANYABIASHARA WANAOFANYA MNADA BARABARANI KURUDI KWENYE SOKO RASMI LA KILOLELI

Posted on: June 5th, 2024

RC MTANDA AWATAKA WAFANYABIASHARA WANAOFANYA MNADA BARABARANI KURUDI KWENYE SOKO RASMI LA KILOLELI


Mhe. Said Mtanda, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amewataka wafanyabiashara wilayani Ilemela kufuata sheria za nchi kwa kufanya shughuli zao kwenye masoko rasmi na Halmashauri isimamie hilo kwa kupunguza Minada ya barabarani na kuhamasisha wabaki kwenye masoko yaliyopangwa.

Ametoa agizo hilo leo tarehe 05 juni, 2024 wakati akizungumza na wafanyabiashara wa Soko la Kiloleli lililopo kwenye kata ya Ibungilo wilayani Ilemela baada ya kubaini wafanyabiashara wadogo kususia Soko hilo lenye miundombinu rafiki na kujikita kwenye magulio ya mnada yanayofanyika kwenye hifadhi za barabara.

"Kukaa kwenye masoko kuna faida kubwa ya kwanza ikiwa ni kutambulika nani yupo wapi na anafanya biashara gani, watu wafuate sheria wakae kwenye masoko sio kuendekeza minada inayofanyika barabarani, tupunguze magulio ili mabenki wajue wanawapata wapi kuwakopesha na hata Mikopo ya Rais Samia ikishakua tayari itakua rahisi kuwapata." Amesisitiza Mhe. Mtanda.

Akibainisha Miradi mikubwa inayotekelezwa Mwanza, Mtanda amesema Soko Kuu la Mjini Kati linalojengwa kwa zaidi ya shilingi Bilioni 20 linaelekea kukamilika na kwa sasa limefikia 95% ya ujenzi na Serikali inatarajia kuongeza Bilioni 3 ndani ya mwezi huu ili likamilike na waganyabiashara zaidi ya elfu mbili watarudi kuendelea na biashara kwenye soko lile la kisasa.

"Nimetoa wito kwa maeneo yote niliyopita kwamba Askari wa Jeshi la akiba kazi yao sio kupiga wananchi na kunyang'anya biashara nasi tutawafikisha mahakamani wanaofanya hivyo bali wanapaswa kukamata na kuwafikisha kwenye vyombo husika." Mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Mhe. Hassan Masala amesema wapo tayari kutekeleza maagizo hayo na kwamba wamejipanga kuboresha miundombinu kwenye masoko yao na kwa mwaka wa fedha unaoendelea wametumia zaidi ya Milioni 180 kukarabati miundombinu kwenye masoko lakini bado machinga wamejikita kufanya biashara kwenye hifadhi za barabara kwa kigezo cha mnada.

Magabe Ligata, mwenyekiti wa Soko la Kiloleli na mwenyekiti wa Wafanyabiashara na Masoko wilayani Ilemela ametoa kwa wafanyabiashara wenzake kurudi kwenye soko hilo ili maeneo ya nafaka, ndizi, matunda na nguo yapate wafanyabiashata kuliko hali ya sasa ya kuwa na wafanyabiashata 386 pekee kwenye soko hilo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti