• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWATAKA WALIOVISHWA NISHANI WAKAWE MABALOZI WAZURI KWA WENGINE

Posted on: June 19th, 2024

RC MTANDA AWATAKA WALIOVISHWA NISHANI WAKAWE MABALOZI WAZURI KWA WENGINE


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewapongeza maafisa, wakaguzi na askari wa Jeshi la Zimamoto waliovishwa nishani na kusema mafanikio yao yatakua chachu kwa wengine kufikia na hata kuzidi viwango vya ubora wa kufanya kazi.

Akizungumza leo katika hafla hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Katibu Tawala Mkoani humo Bw. Balandya Elikana amebainisha heshima hiyo waliyopewa na Rais Samia wana wajibu wa kuja na matokeo chanya ya kufanya kazi kwa weledi na nidhamu.

"Nishani zilizotolewa leo ni kumbukumbu kwa sisi tuliopo na wanaokuja kwamba  hawa ni miongoni mwa waliofanya vizuri hivyo niwatake mkawe mabalozi wazuri kwa wengine".Balandya

Aidha  amelipongeza Jeshi hilo la Zimamoto na Uokoaji kwa kazi nzuri na ya  mfano kwa wengine, amesema  limekuwa likifanya kazi kubwa na nzuri ya kuokoa maisha na mali za watu.

"Hongereni sana. ninatambua na kufarijika na jitihada zinazoendelea kufanyika na mafanikio ya kutia moyo kupitia marafiki wa zimamoto". Mtendaji wa Mkoa


Mara baada ya kuwavisha nishani maafisa, wakaguzi na askari 25 wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa na jirani Kwa niaba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, John Masunga amewataka kudumisha nidhamu kazini.

Aidha Kamishna Jenerali Masunga amewataka wale ambao hawakupata nishani hizo kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kutokata tamaa kwani zoezi hilo halijaishia leo bali kuna nishani nyingi zitaendelea kutolewa.

"Tukachape kazi kwa bidii, tuwe na tabia njema, tuendeleze nidhamu katika vituo vyetu vya kazi, hiyo ndio njia pekee itakayohusika katika kuwafanya mkatunukiwe nishani". Kamishna Jenerali Masunga..

Wakati huo huo Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana mapema leo asubuhi Ofisini kwake amefanya mazungumzo na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji John Masunga.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti