• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AWATAKA WATAALAMU SEKTA YA ARDHI KUWA WAADILIFU

Posted on: February 14th, 2025

RC MTANDA AWATAKA WATAALAMU SEKTA YA ARDHI KUWA WAADILIFU


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewakumbusha wataalam wa Sekta ya Ardhi Mkoa wa Mwanza kuepuka vishawishi vya rushwa, kufuata kanuni, taratibu na sheria za ardhi, na kuhakikisha kila kero au mgogoro wa ardhi unafanyiwa kazi na kufika mwisho ili kujenga imani kwa jamii na Wananchi kuhusu utendaji wa sekta ya ardhi.

Mhe. Mtanda ametoa kauli hiyo mapema leo alipokuwa akifungua kikao kazi cha wataalamu wa sekta hiyo Mkoani Mwanza, Mhe. Mtanda amesema kwa sasa wananchi wengi hawana imani ya utendajikazi na sekta hiyo hivyo wanapaswa kutenda haki na kufanya kazi kwa weledi wa juu.

Mkuu wa Mkoa amesema katika malalamiko ambayo huwa anasikiliza na kutatua kila siku ya Jumanne asilimia themanini ya malalamiko hayo ni ya sekta ya ardhi, hivyo amewataka kuona ukubwa wa tatizo na kulishughulikia ipaswavyo.

“Nimeongea hivyo ili muone ukubwa wa tatizo na changamoto hii imesababishwa kwa asilimia kubwa na wataalam wa ardhi wenyewe kwa kutotimiza majukumu yao”. Amesema Mhe. Mtanda.

Sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa amesisitiza juu ya umuhimu wa kuandaa maandiko pamoja na kuzishirikisha taasisi na mashirika yasiyoya kiserikali, kuwashirikisha wananchi pamoja na kutumia teknolojia rahisi na za kisasa katika upangaji wa miji ili kuharakisha maendeleo yawananchi.

Aidha Mkuu wa Mkoa amemshukuru na kumpongeza kwa dhati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kutoa kiasi cha Shilingi Bilioni 50, na kuipatia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ili zitumike kutekeleza mradi wa kupanga, kupima na kumilikisha maeneo nchini.

“Fedha hizo zilipelekwa kwenye Halmashauri 57 ikiwemo Halmashauri za Mkoa wa Mwanza ambazo ni Jiji la Mwanza (Milioni 800), Ilemela (Bilioni3.5) na Buchosa (Milioni 300), Sengerema (Milioni 200) na vyuo vitatu…”.

Naye Bi. Happyness Mtutwa Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Mkoa wa Mwanza amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kutoa elimu nzuri na ushauri uliolenga kuboresha na kuimarisha sekta ya ardhi Mkoani Mwanza na kuahidi kiwa yale yote aliyoyasema Mhe. Mkuu wa Mkoa yatatekelezwa kwa kiwango cha juu na kwa wakati.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti