• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AYASHUKURU MAKUNDI MBALIMBALI USHIRIKI ZIARA YA RAIS DKT. SAMIA

Posted on: June 30th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda kupitia mkutano alioufanya na Waandishi wa Habari ametoa shukrani kwa makundi mbalimbali ya Viongozi pamoja na wananchi wa Mkoa wa Mwanza kwa ushiriki wao katika ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mkoani Mwanza jini 19 – 21 2025.


Mkuu wa Mkoa amesema ziara ya Rais Dkt. Samia Mkoani Mwanza imekuwa ya mafanikio makubwa kutokana na ushiriki wa Viongozi wa Serikali, Dini, Chama cha Mapinduzi, Makundi mbalimbali kama vile Maafisa Usafirishaji, Machinga na wafanya biashara, walijitokeza kushiriki kikamilifu katika mapokezi na ziara nzima.

“Kwa niaba ya Serikali Mkoani Mwanza nipende kutoa shukrani zangu za dhati kwa Viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Mwanza, kwa ujumla mimi kama Mkuu wa Mkoa nimeridhika na ziara ya Rais kama ilivyokuwa imeandaliwa”. Mhe. Mtanda.


Adha, Mhe. Mtanda amewashukuru sana wananchi wa mkoa wa mwanza kwa mwitikio mkubwa na hamasa kubwa lakini pia amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanya kazi kubwa ya uzinduzi wa daraja, maji na mkutano mzuri wa sungusungu.

“Kwenye mradi wa maji butimba tunawashukuru sana Taasisi na wizara ya maji lakini pia Viongozi wa Wilaya ya Nyamagana na wananchiwa Nyamagana kwa kujaa kwa wingi”. Amesema.


Kadhalika amewapongeza Viongozi na wananchi wa Wilaya ya Magu kwa kufanikisha Tamasha la Utamaduni la bulabo.

Tunawashukuru kwa ushiriki wao na tunaendelea kuomba ushirikiano wao sio tu kwa ziara ya Rais hata kwa viongozi wengine watakaoweza kuja katika Mkoa wa Mwanza maana picha na taswira tulioonesha imeleta matumani kwamba umoja, mshikamano na upendo umetawala mwanza. Amesema Mkuu wa Mkoa.


Kabla ya kuhitimisha mkutano huo Mhe. Mtanda ametoa pongezi pia kwa Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Mwanza kwa mchango wao mkubwa sana katika kuhabarisha na kuhamasisha umma kushiriki ziara ya Mhe. Rais.

“Kwa hiyo ninawapongezeni sana kwa ushiriki wenu, mlitoa habari kwa usahihi na kwa wakati, kazi iliyofanyika ni kubwa sana kwa hiyo tunawashukuru mno”.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti