• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AZINDUA RASMI KAMATI YA USHAURI WA KISHERIA YA MKOA

Posted on: February 17th, 2025

RC MTANDA AZINDUA RASMI KAMATI YA USHAURI WA KISHERIA YA MKOA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameizindua rasmi kamati ya ushauri wa kisheria ngazi ya Mkoa na kutoa wito kwa wajumbe wa kamati hiyo kufanya kazi kwa weledi.

Akizungumza na wananchi waliohudhuria uzinduzi huo leo kwenye viwanja vya Ofisi ya mkuu wa mkoa, Mtanda amesema kuwa kamati hiyo itasaidia wananchi kwa kupata huduma ya kisheria bila malipo.

"Nawaomba sana wajumbe wa kamati hii iliyojaa wataalamu fanyeni kazi kwa weledi, tutawatathmini kuona mnavyowahudumia wananchi", amesisitiza mkuu wa mkoa wakati wa uzinduzi wa kamati hiyo.

Aidha, Mhe. Mtanda amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mpango huo wa kuwasogezea karibu wananchi huduma  hiyo ya kisheria huku migogoro mingi ya ardhi ikiongoza.

"Ofisi yangu kila siku ya Jumanne tunasikiliza kero za wananchi, idadi kubwa ya wananchi wanaofika wanasumbuliwa na migogoro ya ardhi, sasa kamati hii naomba mtambue kuwa sitapenda kuona wananchi wanatoa malalamiko haya kwa viongozi wa juu", ameongeza.

Ametoa pia maelekezo kwa wakuu wote wa Wilaya mkoani Mwanza kwenda kuziunda kamati hizo ngazi za wilaya ambazo zitashirikiana na kamati ya Mkoa kutatua kero za wananchi.

Akitoa taarifa fupi kuhusiana na kamati hiyo, mwakilishi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bi. Neema Ringo amesema zaidi ya kesi 500 kwa mwaka wanazipokea za wananchi kuishtaki Serikali, hivyo kuundwa kwa kamati hiyo itapunguza kesi hizo.

Mpango huo ulizinduliwa rasmi Machi 21, 2024 na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti