• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AZITAKA HALMASHAURI KUTENGA ARDHI KWA AJILI YA KUJENGA MAKAZI YA WAZEE

Posted on: June 10th, 2024

RC MTANDA AZITAKA HALMASHAURI KUTENGA ARDHI KWA AJILI YA KUJENGA MAKAZI YA WAZEE


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amezitaka Halmashauri Mkoani humo kutenga maeneo maalum katika mpango wa matumizi bora ya ardhi na kuhakikisha wanajenga makazi ya kulea wazee ili kuwahakikishia huduma bora.

Mhe. Mtanda ametoa rai hiyo wakati akizungumza na jumuiya ya wazee wa wilaya ya Sengerema katika mkutano wake alioufanya leo Juni 10, 2024 alipofanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo na kuzungumza na makundi mbalimbali wilayani humo.

"Sisi ni wazee watarajiwa, mipango yote tutakayoweka itatusaidia wenyewe siku za usoni hivyo ni lazima sasa tutenge maeneo ya kujenga makazi ya malezi na mwakani tuanze ujenzi ili wazee wakae sehemu moja na tupeleke huduma za kijamii." Mkuu wa Mkoa.

Aidha, amesema katika kuhakikisha wazee wanakua na malezi bora ni lazima familia iwajibike kuwatunza na watoto wawalee wazee maana wao tayari wamelelewa na kusomeshwa vizuri hadi kufika hapo walipo hivyo ni lazima wathamini upendo huo ambao pia unasisitizwa na maandiko ya dini.

Vilevile, ametoa wito kwa watumishi wa afya kuhakikisha wanatoa huduma za afya kwa wazee bila malipo kwa mujibu wa sera zetu na amezitaka familia kuhakikisha malezi ya mtoto yanaanza kwenye unyonyeshaji wa maziwa ya mama kwa zaidi ya miaka miwili na nusu ili kuwahakikisha afya njema.

Halikadhalika, amewataka wazee kuendelea kumuunga mkono Rais Samia kwa kumuombea awe na afya na siha njema kwani anaonesha kwa vitendo upendo wake kwa kundi hilo kwa kuwaboreshea huduma za afya ikiwepo uwepo wa madirisha ya wazee ya kuwahudumia kwa kipaumbele.

Mhe. Hamis Tabasam, Mbunge wa Sengerema amesema kuwa Jumuiya ya Wazee wilayani humo ina jumla ya wajumbe 640 na kwamba adha kubwa wanayoipata kwenye huduma za jamii ni gharama kubwa za matibabu hivyo wanaomba kupatiwa bima za afya.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti