• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AZITAKA HALMASHAURI KUTOA FEDHA ZA LISHE MASHULENI

Posted on: August 22nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amezitaka Halmashauri Mkoani humo kuhakikisha wanapeleka fedha za lishe kwenye shule kwa ajili ya kununua virutubisho na chakula dawa cha watoto kwa mujibu wa bajeti zao .

Ametoa wito huo mapema leo agosti 22, 2025 wakati akifungua kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa Lishe kwa kipindi cha mwezi Julai hadi Juni 2024/25 kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amesema Wakurugenzi ni lazima watimize wajibu wa kutenga bajeti na kupeleka fedha za masuala ya lishe shuleni kwa ajili ya kutekeleza afua za lishe kwa watoto ili kujenga taifa lisilo na utapia mlo na udumavu.

Aidha, amezipongeza Halmashauri za Buchosa, Ilemela, Kwimba, na Sengerema kwa kupeleka fedha hizo na kupelekea mkoa kuwa na wastani wa aslimia 92 katika kishiria hicho.

Kadhalika, amezitaka Halmashauri zilizofanya chini ya ufanisi wa wastani huo vizuri na kukwamisha kufikia malengo kuongeza juhudi kuhakikisha hawaurudishi nyuma mkoa kwenye masuala ya lishe.

Katika kufanikisha afua hiyo, Mhe. Mtanda amewataka idara ya Elimu kuhamasisha wazazi na walezi kutoa michango kwa ajili ya kufanikisha upatikanaji wa chakula kwa watoto shuleni na amezitaka shule zenye mashamba kulima mazao ya lishe kwa ajili ya kuongeza virutubisho kwenye chakula wanachopatiwa watoto.

Vilevile, ametumia wasaa huo kuwataka viongozi na watendaji kwenda kuhamasisha wananchi waweze kushiriki katika uchaguzi Mkuu wa mwezi Oktoba 2025 kwa amani na utulivu.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti