• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA NA BALOZI WA ITALIA TANZANIA WAKUBALIANA KUANDAA KAMBI YA MATIBABU

Posted on: October 2nd, 2024

RC MTANDA NA BALOZI WA ITALIA TANZANIA WAKUBALIANA KUANDAA KAMBI YA MATIBABU


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewasilisha ombi kwa Balozi wa Italia nchini Tanzania Mhe. Giuseppe Sean Coppola la kuanzisha kambi maalumu ya matibabu Mkoani humo, ombi ambalo limekubaliwa na Balozi huyo anbaye amesema litaratibiwa na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando.

Mhe. Mtanda ametoa ombi hilo leo Oktoba 02, 2024 wakati akizungumza mara baada ya kumpokea Balozi huyo Ofisini kwake, aliyewasili Mkoani humo kushiriki Kongamano la pili la Kudhibiti Saratani Duniani lililoandaliwa na kuratibiwa na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando na kufanyika katika Ukumbi wa Malaika Hoteli Wilayani Ilemela.

Mhe. Mtanda amesema Mkoa wa Mwanza ni Mkoa mkubwa wenye idadi ya watu wengi baada ya Mkoa wa Dar es Salaam hivyo kuanzisha kambi hiyo itasaidia kuondoa kadhia kwa watu wenye uchumi mdogo ambao wamekuwa wakisumbuliwa na maradhi mbalimbali na kushindwa kupata matibabu kutokana na kushindwa kumudu gharama za tiba.

Aidha Mhe. Mtanda pia amemtaka Balozi huyo kuleta wawekezaji ambao watasaidia katika kuanzisha viwanda vya chakula cha samaki na kusambaza vyakula hivyo kwa wafugaji wa samaki wa vizimba ambao kwa sasa wamekuwa wakikabiliwa na uhaba wa chakula.

"Kama utatusaidia tukapata wawekezaji wazuri katika viwanda vya chakula cha samaki nina imani utakuwa umetusaidia sana". Mhe. Mtanda.

Naye Balozi huyo wa Italia amesema kuhusu suala la huduma ya kambi ya matibabu wanaweza kuanza kwa kufanya walau mara moja kwa mwaka na baadae wakaendelea, Aidha pia amemhakikishia Mhe. Mtanda pia kuhusu suala la wawekezaji amelichukua kwa utekelezaji.


Sambamba na hayo Mhe. Balozi Coppola amesema yuko tayari kushirikiana na Serikali ya Mkoa katika masuala ya utalii, madini na kwamba kwa wakati wowote yeye na timu yake watatoa ushirikiano wa kutosha.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Nchi ya Italia imekuwa na mahusiano ya pande mbili yenye mizizi ya kina tangu kuimarishwa kwa uhusiano rasmi wa kidemokrasia mwaka 1970 ambapo Tanzania ilifungua rasmi Ubalozi wake Roma mwaka 1972 huku Ubalozi wa Italia ukifunguliwa rasmi nchini Tanzania mwaka 1961.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti