• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA: UZINDUZI MV MPUNGU NI ISHARA YA MAENDELEO SEKTA YA USAFIRISHAJI MAJINI

Posted on: May 21st, 2025

RC MTANDA: UZINDUZI MV MPUNGU NI ISHARA YA MAENDELEO SEKTA YA USAFIRISHAJI MAJINI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Said Mtanda amesema uzinduzi wa wa Meli kubwa ya mizigo ya MV Mpungu yenye uwezo wa kubeba tani 1,000 sawa na magari ya kubeba mizigo (Trailer 21) ni ishara ya maendeleo na ukuaji wa sekta ya usafirishaji majini katika Mkoa wa Mwanza.

Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo leo mei 21,2025 wakati wa uzinduzi wa Meli hiyo ya MV Mpungu uliofanyika katika Bandari ya Mwanza Kusini ambapo amesema kuzindua meli hiyo katika Mkoa wa Mwanza ni uamuzi sahihi kwa kuwa ni Mkoa wa Kimkakati na kiuchumi.

“Ni matarajio ya wengi kuwa kuzindua kwa meli hii kubwa ya mizigo ya MV Mpungu itakata kiu ya Wafanyabiashara waliokuwa wakisubiri kwa hamu meli kubwa ya kusafirisha mizigo kutoka Mwanza kwenda Portbell, Uganda”. Amesema.

"Uwepo wa meli hii utachangia kukua kwa sekta ya usafirishaji majini na kukua kwa pato la Taifa." Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Kadhalika, Mkuu wa Mkoa amesema juhudi kubwa sana zimefanywa na Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha usafiri wa majini kwa ujenzi wa vivuko vitano (5) vyenye thamani ya Sh. Bilion 28.

Pia amesema serikali imetoa fedha takribani shilingi Bilioni 18.6 kugharamia mradi wa upanuzi wa Bandari ya Mwanza Kaskazini ambao umefikia Asilimia 58. Ujenzi wa Meli Mpya ya MV Mwanza itakayogharimu 123 Bilioni, yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200, tani 400 za mizigo magari madogo 20 na malori 3, mradi umefikia asilimia 98.

“Lakini pia tuna ujenzi wa Makao Makuu ya Kituo cha Utafutaji na Uokozi katika Ukanda wa Ziwa Viktoria (MRCC –Regional Maritime Rescue Coordination Centre), unaogharimu 64.99 Bilioni na umefikia Asilimia 84”. Amefafanua.

Akisoma taarifa kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka za Bandari, Meneja wa Bandari Ziwa Victoria Bw. Erasto Ligenge amesema bandari ya Mwanz kusini ni moja ya vituo muhimu vya kimakakatu ambapo ina uwezo wa kuhudumia tani laki mbili kwa mwaka.

Aidha, amesema uzinduzi wa meli hiyo mpya ya mizigo itasaidia kubeba mizigo mingi kwa wakati mmoja ambapo kwa safari moja mizigo zaidi ya tani moja itasafirishwa kadhalika itapunguza safari za muda mrefu kwa njia ya barabara pamoja na kushusha wastani wa gharama za usafirishaji.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti