• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MWANZA ASIKILIZA KERO ZA WAMACHINGA,VIONGOZI WA MASOKO NA MINADA MKOANI MWANZA

Posted on: September 14th, 2023

RC MWANZA ASIKILIZA KERO ZA WAMACHINGA,VIONGOZI WA MASOKO NA MINADA MKOANI MWANZA


*Awataka Machinga kufanya biashara kwenye maeneo waliyopangiwa*


*Aaagiza kuwepo dawati la kusikiliza kero za wafanyabiadhara kila Halmashauri*


*Aitaka LATRA kuweka utaratibu wa mizunguko ya mabasi kwenye masoko ili kuwe na muingiliano wa watu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla amekutana leo viongozi wa makundi ya wafanyabiashara kwa lengo la kusikiliza kero zao na kutoa maagizo kumi likiwemo la kuwasisitiza kufanya biashara zao kwenye maeneo waliyopangiwa huku mikakati ya kuboresha maeneo yao ikiendelea kufanyiwa kazi.

Akizungumza na makundi ya wawakilishi hao kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ametoa maagizo likiwemo la kuzitaka Halmashauri zote Mkoani humo kuwa na dawati la kusikiliza kero za wafanyabiashara hao ambalo litasaidia kuzitatua changamoto zinazowakabili za mara kwa mara.

Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ana uzoefu na changamoto za wafanyabiashara kutokana na kufanya kazi kwenye majiji kadhaa nchini amewaagiza kila Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi na Maafisa biashara kuweka mpango mkakati wa kuboresha masoko katika maeneo yao.

"Nawaagiza pia LATRA kuhakikisha wanaweka mpango wa mizunguko ya mabasi kupita kwenye masoko yote ili kuwepo na muingiliano wa watu na biashara iweze kufanyika kwa tija, haiwezekani kuwaweka wafanya biashara kwenye maeneo ambayo hakuna muingiliano wa watu, wataishia kuyakimbia masoko wakihofia mitaji yao kukatika, LATRA mzingatie hilo,"CPA Makalla.

Kuhusu miundombinu Mkuu huyo wa Mkoa ametoa agizo kwa TARURA kuboresha barabara zote maeneo ya masoko ili kuhakikisha zinapitika kwa urahisi ili shughuli za kupeleka mizigo na wanunuzi zifanyike kwa wepesi.

Aidha, Makalla amewakumbusha Wakuu wa Wilaya kuwa na vikao vya mara kwa mara na wafanyabiashara hao hali ambayo itasaidia kuzitambua kero zao na kuzipatia ufumbuzi kwa haraka.


Kuhusu Soko kuu lililopo katikati ya Jiji linalotarajiwa kukabidhiwa kwa Serikali Disemba mwa mwaka huu, Mhe.Makalla amewahakikishia kipaumbele kitatolewa kwa wafanyabiashara wa awali ambao walikuwepo kabla ya kupisha mradi huo kufanyika.

Vilevile, Mkuu huyo wa Mkoa ametoa rai kwa wafanyabiashara hao kuwa na umoja na kudumisha amani katika shughuli zao na amewaahidi kuwa na vikao nao vya mara kwa mara ili kusikiliza changamoto zao na kuzifanyia kazi.

"Mhe.Mkuu wa Mkoa Wilaya yangu Ina jumla ya wafanyabiadhara 12,850 na masoko 15 licha ya changamoto za hapa na pale lakini biashara zao tunahakikisha zinafanyika katika mazingira mazuri," Amesema Mhe.Amina Makilagi,Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana.

."Wilaya ya Ilemela tuna jumla ya wafanyabiashara 3500 na masoko 8 yaliyo rasmi na yasiyo rasmi lakini tumekuwa makini kuhakikisha wafanyabiashara hao wanatii bila shuruti miongozo iliyopo,"Mhe.Hassan Masala, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti