• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC Shigella ayafunga maonesho ya Nanenane Mwanza na kutoa Rai kwa washiriki kuyatumia kuelimika

Posted on: August 8th, 2022

Maonesho ya Nanenane Mkoani Mwanza yamefungwa rasmi leo agosti 08, 2022 huku rai ikitolewa kwa washiriki hao kutumia Elimu waliyoipata kutoka kwa wadau mbalimbali wa Kilimo na mifugo kama njia ya kuzidi kuongeza tija kwenye mazao na kuboresha shughuli zao.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martin Shigella katika hotuba yake ya Ufungaji kwenye Viwanja vya Nyamhongolo amesema kwenye maonesho hayo kuna fursa za kuonana na Wataalam mbalimbali kuanzia Kilimo na masuala ya fedha ambao watamsaidia mkulima au mfanyabiashara kufanya kazi kwa ufanisi.

"Haya ni maonesho yangu ya kwanza kushiriki nikiwa Mkuu wa Mkoa wa Geita nimeyazungukia mabanda na kushuhudia fursa nyingi ambazo zikitumiwa vizuri zitainua uchumi wa washiriki." Mkuu wa Mkoa Geita

Mhe. Shigella amebainisha kuwa, hakuna sababu ya mfugaji kujivunia wingi wa Ng'ombe wakati hawamnufaishi ipasavyo kutokana na kukosa ushauri wa kitaalamu hivyo huu ni wakati wa kubadilika.

Akimkaribisha katika ufungaji huo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Adam Malima amesema kuna kila sababu ya kuyaboresha maonesho hayo hasa baada ya kushuhudia hamasa kubwa ya wananchi na washiriki.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya maonesho ya Nanenane Mkoa Emil Kasagara amebainisha maonesho hayo yamekuwa na muitikio chanya kila mwaka kutokana na maandalizi bora wanayofanya.

Kwa upande wa washindi wa zawadi kwa Washiriki Wilaya ya Magu imeonesha kuibuka kimasomaso kutokana na zawadi nyingi kwenda kwa Washiriki kutoka wilayani humo.

Maonesho ya Nanenane Kanda ya Ziwa Magharibi yameshirikisha Mikoa ya Geita,Kagera na mwenyeji wao Mwanza.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti