• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

REDIO ZA JAMII ZATAKIWA KUELIMISHA UMMA KUFAHAMU MFUMO WA M-MAMA

Posted on: November 8th, 2024

REDIO ZA JAMII ZATAKIWA KUELIMISHA UMMA KUFAHAMU MFUMO WA M-MAMA


Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba ametoa wito kwa Redio za jamii kusaidia kuelimisha umma juu ya mfumo wa M-Mama unaotoa fursa ya usafiri wa dharula kwa Mama na Mtoto mchanga kuanzia kwenye ngazi ya jamii hadi kwenye vituo vya kutolea huduma wakati wa dharula.

Akifungua semina ya mafunzo kwa Redio za jamii kutoka mikoa ya kanda ya ziwa kwenye hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza leo Novemba 08, 2024 Dkt. Lebba amesema wanahabari kutoka kwenye Redio za kijamii wana nafasi kubwa ya kusaidia wananchi kuweza kufahamu mfumo huo ulioletwa mahsusi kwa ajili ya kuokoa maisha.

Ameongeza kuwa katika tafiti zilizofanyika imeonekana kumekua na ucheleweshaji wa taarifa, miundombinu duni ya kufika kwenye vituo vya kutolea huduma pamoja na ucheleweshaji kwenye kupatiwa huduma mara wafikapo wagonjwa hospitali hivyo mfumo huo umekuja na suluhisho kwenye adha hizo.

"Ndugu washiriki, tangu kuanza kwa mfumo huu mpaka sasa zaidi ya dharula elfu 98 zimesafirishwa na kwa Mwanza pekee ni zaidi ya dharula elfu 6 kwa wastani wa 300 kwa mwezi zimefikiwa."

Amefafanua Dkt. Lebba.

Aidha, mganga huyo wa mkoa amezitaka halmashauri kuhakikisha magari ya wagonjwa (Ambulance) yanakua tayari kutoa huduma wakati wote pamoja na kulipa kwa wakati kwa madereva ngazi ya jamii kwa mujibu wa mkataba yaani ndani ya siku 14 tangu watoe huduma wawe amelipwa.

"Naamini redio zetu mtatusaidia sana kuelimisha jamii kuwa huduma hii inapatikana kuanzia ngazi ya jamii na kwenye vituo vya kutolea huduma, matumizi sahihi ya namba 115 kwa ajili ya kuwaokoa wajawazito pamoja na watoto wachanga." Amesema Mganga Mkuu.

Awali, Mratibu wa mfumo wa M-Mama kutoka Mkoa wa Mwanza Stanley Kajuna amesema kuwa walengwa waliokusudiwa zaidi ni mama mjamzito, mama aliyejigungua mpaja siku 42, mtoto mchanga hadi siku 28 na jamii kwa ujumla na kwamba tayari kuna madereva 4000 wamesajiriwa.

Katika kusaidia jamii, Mfumo wa M-Mama unachagizwa na kaulimbiu isemayo M- Mama Okoa maisha na inaendeshwa bila malipo yoyote kwa wateja kuanzia kwenye simu hadi usafiri wa kwenda kwenye kituo cha kupata huduma za afya.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti