• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RMO MWANZA ATAKA UBUNIFU KUFIKISHA ELIMU YA MALEZI, MAKUZI KWA JAMII

Posted on: August 19th, 2025

Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba ametoa wito kwa wadau wa Malezi mkoani humo hususani wajumbe wa mkakati wa kutokomeza ukatili wa kijinsia kuwa wabunifu katika kuhakikisha wanafikisha elimu hiyo kwa jamii kwa ajili ya ustawi wa jamii.

Ametoa wito huo mapema leo Agosti 19, 2025 wakati akifungua mkutano wa maandalizi ya kikao cha malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto kitakachofanyika mapema mwezi Septemba 2025 chini ya uongozi wa Katibu Tawala wa Mkoa.


Amewataka wadau hao kuhakikisha wanatumia fursa ya ratiba ya wizara ya mwezi huo wa uelimishaji unaoambatana na wiki ya ustawi wa jamii kwenda kutoa elimu kwenye jamii kwa kutumia mbinu mbalimbali kama redioni na mikusanyiko vijijini kuhusiana na malezi na ukatili wa kijinsia kabla ya kuchukua sheria kwa wakaidi.

Amesema serikali imeweka afua tano kuhakikisha makuzi, malezi na maendeleo ya mtoto yanakua na ustawi na kwamba programu mbalimbali zinazosawili afua hizo yanapaswa kuzingatiwa kwa gharama yoyote ili mwisho wa siku jamii iwe salama.

Vilevile, ametumia wasaa huo kuwashukuru wadau wote pamoja na kumpongeza Afisa Ustawi wa Jamii wa Mkoa pamoja na wasaidizi wake kwa uchapakazi kwani Mwanza imepiga hatua kubwa katika kuelimisha na kupunguza matendo ya ukatili kutokana na juhudi zao za kuhakikisha elimu ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto inawafikia wananchi.

Akitoa salamu za Wizara ya maendeleo ya Jamii Idara ya Mtoto bi. Mery Shila amesema wizara hiyo kwa kushirikiana na mikoa wanahakikisha mtoto kuanzia mwaka mmoja hadi minane analindwa na jamii nzima na ndio maana wanasukuma afua mbalimbali za malezi.

Aidha, amebainisha kuwa viongozi wa dini kote nchini wamekua kiungo kikubwa kwenye malezi ya watoto kwa kutoa malenzi na mafundisho ya kiroho katika kuhakikisha wanakua na tabia njema ili ikiwezekana madawati ya jinsia yakose mashauri ya ukatili.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti