• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

SERIKALI ITAENDELEA KUTOA VIFAA TIBA ILI KUBORESHA SEKTA YA AFYA:RC MTANDA

Posted on: November 22nd, 2024

SERIKALI ITAENDELEA KUTOA VIFAA TIBA ILI KUBORESHA SEKTA YA AFYA:RC MTANDA


Katibu Tawala Msaidizi Rasilimali watu na Utawala Bw.Daniel Machunda amefunga mkutano wa umoja wa Wahandisi na mafundi sanifu vifaa tiba kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuwahakikishia Serikali ya awamu ya sita itaendelea kutoa ushirikiano na marafiki wa maendeleo ili kuboresha sekta ya afya.

Akizungumza leo Novemba 21,2024 na washiriki wa mkutano huo wa saba wa siku mbili kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwenye ukumbi wa mikutano Malaika wilayani Ilemela Jijini Mwanza,Machunda amesema Serikali inatambua mchango wa Taasisi mbalimbali zinazojihusisha na afya hivyo ushauri na mapendekezo yote yaliyoazimiwa kwenye mkutano huo yatafanyiwa kazi.

"Ndugu washiriki awali ya yote nichukue nafasi hii ya kumshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi kuboresha sekta hii hapa nchini,mfano mzuri ni hapa Mwanza miradi mingi ya afya tunayo na ipo katika hatua nzuri,"Machunda.

Ameongeza kuwa mkutano huo umewajumuisha Wahandisi wa vifaa tiba kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki lengo likiwa ni kuhakikisha kunakuwa na hatua kubwa ya utolewaji wa huduma bora kwa wananchi.

Kwa upande wake Rais wa Umoja wa vyama vya Wahandisi na mafundi sanifu wa vifaa tiba Afrika Mashariki (FEAHEA) Mhandisi Costica Witonze amebainisha siku mbili za mkutano huo wameangalia changamoto, wamejadiliana na kupendekeza mkakati mwafaka wa kuboresha sekta hiyo hasa eneo la vifaa tiba.

"Ndugu mgeni rasmi tunatambua umuhimu wa sekta hii,ingawa zipo changamoto mbalimbali za kifedha kwa nchi za Jumuiya hii katika kufikia malengo tuna imani baada ya mkutano huu tutakuwa na maazimio chanya yatakayosaidia kusonga mbele",Rais wa Jumuiya ya Wahandisi.

Mkutano huo uliobeba kauli mbiu ya "Upatikanaji wa hewa tiba ya Oksijeni na Usimamizi wa vifaa tiba ni chachu ya huduma bora za afya",nchi ya Rwanda watakuwa wenyeji wa mkutano ujao.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti