• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

SERIKALI MKOA WA MWANZA KUENDELEA KUWAUNGA MKONO WAFANYABIASHARA WAKUBWA NA WADOGO

Posted on: February 6th, 2025

SERIKALI MKOA WA MWANZA KUENDELEA KUWAUNGA MKONO WAFANYABIASHARA WAKUBWA NA WADOGO


Serikali Mkoa wa Mwanza imedhamiria kuwaunga mkono Wafanyabiashara mbalimbali Wakubwa na wadogo wanaopatikana katika Mkoa huo kwa kuwa Serikali ya Rais Samia inathamini mchango wao katika kukuza uchumi wa nchi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda alipokuwa akizungumza katika hafla ya kuitambulisha Kampuni ya AI Mansour Auto Tanzania, Isuzu East Africa na MRC Motors ambao ni wauzaji wa magari mapya ya Isuzu Jijini Mwanza.

Mkuu wa Mkoa amesema Serikali ya Rais Samia imeimarisha uchumi na usalama kwa hali ya juu na amewatoa hofu Wafanyabiashara hao kuwa na amani hata wakileta magari zaidi ya mia tano Mkoani Mwanza wajue kuwa yapo sehemu salama.

Aidha Mkuu wa Mkoa amesema kampuni hiyo ya Isuzu kuja kuwekeza katika Mkoa wa Mwanza hawajafanya makosa kwani ni mkoa wa kimkakati na wenye idadi kubwa ya watu ukiwa pia ni kitovu cha uchumi wa Mikoa 7 ya Kanda ya Ziwa.

“Nyie wenyewe kupitia Bwana Ochieng mmekiri kwamba hata mteja wenu wa kwanza alitoka Mkoa huu kwa iyo mnapofanya Mwanza kama sehemu yenu ya biashara nyie ni wachumi wazuri na mnafahamu kuhusu soko lilipo”.

Sambamba na hayo ametoa wito kwa Wananchi kutembelea ofisi za Isuzu Mwanza ili waweze kupata huduma za magari na sasa si lazima kwenda Dar es Salaam yameletwa hapa na kizuri zaidi wanauza magari toleo la kwanza na sio yale yaliyotumika.

Naye Mkurugenzi wa Wateja kutoka Kampuni ya Isuzu Afrika Mashariki Bw. Kelvin Ochieng amesema Isuzu ni kampuni inayothamini wateja wake na kwa miaka 5 tangu kuanzishwa kwake wameshauza magari zaidi ya 1200.

Aidha amesema kwa hapa Mwanza wamekuwa wakiungwa mkono na wadau wengi kutoka makampuni na mashirika mbalimbali ya serikali na kuwataka Wafanyabiashara na wadau kuwaunga mkono.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti