• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

SERIKALI YABORESHA HUDUMA ZA SARATANI YA MATITI MWANZA

Posted on: October 22nd, 2025

Serikali kwa kushirikiana na Shirika lisilo la Kiserikali la Jhpiego imeendelea kuboresha huduma za matibabu ya saratani ya matiti Mkoani Mwanza kupitia Mradi wake wa Beat Breast Cancer awamu ya pili unaodhaminiwa na PFIZER Foundation ambao unalenga kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huo kwa kuimarisha uchunguzi wa mapema na upatikanaji wa matibabu.


Akizungumza leo Oktoba 22, 2025 na waandishi wa habari ofisini kwake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dkt. Jesca Lebba ameipongeza serikali kwa hatua hiyo muhimu na kuishukuru kwa kuuchagua Mkoa wa Mwanza kuwa miongoni mwa wanufaika wa awamu ya pili ya mradi huo.


Dkt. Lebba amewataka wananchi wa Mkoa wa Mwanza kuchangamka kwa kujitokeza kwa wingi katika vituo vya kutolea huduma za afya ili waweze kuchunguza afya zao na kupatiwa matibabu.

“Tutahakikisha tunawafikia wananchi wa maeneo yote na nitoe rai kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kuja kuchunguza afya zao na kupatiwa huduma za uchunguzi, ushauri na matibabu”.


Ameongeza kuwa changamoto kubwa ambayo wanakutana nayo ni uelewa mdogo wa jamii juu ya dalili na matibabu ya saratani ya matiti, watoa huduma wachache pamoja na vituo vya kutolea huduma hiyo ya vipimo na elimu juu ya ugonjwa huo.


Aidha, amesema wameweza kufanya uchunguzi kwa wanawake zaidi ya 23,000 na kuanzia mwezi Januari mpaka Septemba mwaka huu wananchi 46 wamebainika kuwa na saratani ya matiti na kati yao 27 wameshaanza kupatiwa matibabu na wengine wapo katika ushauri nasaha.


Naye Daktari Bingwa wa Upasuaji kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou-Toure Dkt. Jackson Chiwaligo amewasisitiza wanawake kujifanyia uchunguzi wa awali ili waweze kutambua mabadiliko katika miili yao, huku akitoa wito waweze kufika hospitali pale ambapo watahisi mabadiliko yoyote katika matiti.

Mkoa wa Mwanza ni miongoni mwa Mikoa minne kwa Tanzania bara ambayo inanufaika na mradi wa PFIZER-BREAST CANCER na kutoa huduma ya kupima na kutibu saratani ya matiti ukiwa na vituo 32 zikiwemo Hospitali ya Kanda, Hospitali ya Rufaa, Hospitali za Wilaya na Halmashauri huku ikifanikisha kutoa elimu kwa watoa huduma 60.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti