• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

STORI YA BABA NA WATOTO WATATU WALIOKUMBWA NA UGONJWA WA KUTETEMEKA NA KUPOOZA MWILI YAMGUSA RC MTANDA

Posted on: February 12th, 2025

STORI YA BABA NA WATOTO WATATU WALIOKUMBWA NA UGONJWA WA KUTETEMEKA NA KUPOOZA MWILI YAMGUSA RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Februari 12, 2025 amefika katika Mtaa wa Ibanda - Mkolani Wilayani Nyamagana kwenye familia ya Mzee Frednand Zephania yenye wanafamilia 4 wanaosumbuliwa na maradhi ya kutetemeka pamoja na kupooza mwili na kisha kuwapatia msaada.

Amesema alipata mfadhaiko sana baada ya kuona taarifa hiyo kwenye vyombo vya habari na akaagiza wasaidizi wake kufuatilia tatizo ni nini lakini pia mahitaji ya kuweza kuwasaidia familia hiyo na ndipo amefika kuona namna gani watapata matibabu.

Mhe. Mtanda mara baada ya kupata taarifa kamili kutoka kwa wasaidiizi wake ndio akaamua kutafuta namna ya kupata bima za afya kwa wagonjwa zitakazowasaidia kupapatiwa matibabu bila ya kulipa kiasi chochote.

 “Bima hizi zina jumla ya gharama za shilingi milioni 2.1 ili kuwapunguzia mzigo wa gharama za matibabu ambapo mlikuwa mnalazimika kulipa fedha taslimu”. Amesema Mhe. Mtanda.

Sambamba na bima hizo, Mkuu wa Mkoa ameipatia familia hiyo mtaji wa biashara wa shilingi milioni tano (5) ili kusaidia mahitaji ya kila siku kama chakula na mahitaji mengine ya kila siku.

Katika hatua nyingine, Mhe Mtanda amemuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza kuwapatia familia hiyo kibanda cha kufanya biashara katika soko jipya la mjini kati ili mwanafamilia mmoja ambaye hajaathirika na changamoto hiyo aweze kufanya biashara na kumudu kuhudumia familia hiyo.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wadau mbalimbali watakaoguswa na changamoto iliyoikumba familia hiyo kusaidia kuongeza mtaji kwa wanafamilia hao ili waweze kupata mtaji mkubwa zaidi huku akimtaka Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba kuwapa kipaumbele wakati wote watapohitaji huduma za dharula wapate usafiri mara moja.

Vilevile, Mkuu wa Mkoa ameitaka jamii kuwapa moyo na kuendelea kuisaidia familia hiyo ili waweze kupata faraja kwa changamoto wanayopitia.

Mke wa Mzee Zephania Bi. Bahati Makalle amebainisha kuwa katika nyakati tofauti Mumewe na watoto wake watatu wamepatwa na ugonjwa huo wa kutetemeka na kupooza mwili, aidha alifanya jitihada za kuwapeleka kwenye uchunguzi na kuonesha wana shida ya misuli.

Katika kumudu maisha binti wa mwisho aitwaye Basilisa Zephania alikua anafanya biashara lakini aliifunga kutokana na kuhitajika kumsaidia mama yake kuwauguza wanafamilia hao ambao ni Samson zephania, Judith zephania, Nathan Zephania pamoja baba yao mzee Zephania.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amesema waliunda timu ya wataalamu kuchunguza chanzo cha tatizo hilo ambalo kwa awali wamebaini matatizo ya misuli na kwamba wanaendelea kufuatilia ili kubaini chanzo hasa ni nini.

Sambamba na hilo Dkt. Lebba pia  amewatoa hofu majirani wanaoishi kwenye mtaa huo kuchangamana na familia hiyo kwani uchunguzi wa kitaalamu unaonesha maradhi yanayowasumbua siyo ya kuambukiza.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti