• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

TFDA Yatoa mafunzo kwa wanahabari Mkoa wa Mwanza na Shinyanga

Posted on: May 22nd, 2018


Imeelezwa kuwa afya ya watumiaji bidhaa mbalimbali zitalindwa na kuboreshwa ikiwa sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi sura 219, itasimamiwa na kutekelezwa ipasavyo huku vyombo vya habari vikitimiza wajibu wao kwa usahihi.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Habari Maelezo Zamaradi Kawawa katika kikao kazi cha Wahariri na Waandishi wa Habari kutoka mikoa ya Mwanza na Shinyanga kuhusu uhamasishaji wa sheria ya Chakula,Dawa na Vipodozi sura 219 kilichoandaliwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kilichofanyika mkoani hapa.

Kawawa alisema, wahariri na waandishi wa habari wanamchango mkubwa katika kuhimiza utekelezaji wa sheria hiyo,kuelimisha umma kwa kuwapatia taarifa sahihi zinazohusu shughuli za udhibiti wa bidhaa hizo kutoka vyanzo mbalimbali sambamba na kuijua sheria hiyo.

Alisema, vyombo hivyo vinawajibu wa kutumia kalamu zao kuleta mabadiliko chanya katika jamii kuhusu udhibiti wa bidhaa,kuielimisha juu ya kuzingatia ubora na usalama wa bidhaa hizo pamoja na kuwaibua watu wanaovunja sheria hiyo kwa kutoa taarifa TFDA na kwa vyombo vingine vya sheria vinavyohusika na udhibiti.

“Wana habari waendelee kutoa elimu kwa jamii juu ya madhara watakayo yapata kiafya endapo watatumia bidhaa za chakula,dawa,vipodozi,vifaa tiba na vitendanishi ambayo vipo kinyume na sheria sambamba na kutoa mapendekezo kwa TFDA juu ya namna ya kuboresha usimamizi na utekelezaji wa sheria,”alisema Zamaradi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu TFDA Agnes Kijo alisema,suala la afya ni la jamii nzima,hivyo ni wajibu wakila mtu katika kudhibiti bidhaa bandia na duni,huku waandishi wakiendeleza ushirikiano na mamlaka hiyo katika kuibua wafanyabiashara ambao siyo waaminifu wanaouza bidhaa zilizopita muda.

Kijo alisema, kwa mwaka wanatumia zaidi ya milioni 100 katika kufanya opareshini na ukaguzi maalum wa kudhibiti bidhaa hizo,hivyo ni vyema wananchi wakahamasishwa na kuelimishwa kuacha kutumia ili fedha hizo zitumike kwenye miradi ya maendeleo.

Naye Mwanasheria Mshauri wa TFDA Iskari Fute alisema,madhumuni ya sheria ni kuweka mfumo thabiti wa usalama,ubora na ufanisi wa chakula,dawa,vipodozi,vifaa tiba, vitendanishi,vifaa vya maabara na dawa zenye asili ya miti shamba pamoja na kulinda afya ya jamii ili kutekeleza msingi wa haki ya kuishi.

Hata hivyo Mkurugenzi wa Dawa na Bidhaa Nyongeza wa TFDA Adam Fimbo alisema, bidhaa wanazodhibiti ni zile zenye athari moja kwa moja katika afya ya binadamu,hivyo waandishi wa habari wanamchango mkubwa wa kuelimisha jamii kuhusu matumizi sahihi ya bidhaa hizo.

Aidhaa baadhi ya washiriki wa kikao hicho,waliitaka mamlaka hiyo kufika hadi maeneo ya vijijini kutoa elimu kuhusu madhara yatokanayo na utumiaji wa vipodozi vyenye viambato vyenye sumu na bidhaa bandia na duni.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti