• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

TIMU YA UFUATILIAJI MRADI WA HOSPITALI YA RUFAA UKEREWE YATINGA SITE

Posted on: February 8th, 2025

TIMU YA UFUATILIAJI MRADI WA HOSPITALI YA RUFAA UKEREWE YATINGA SITE


Tarehe 27 Desemba, 2024 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda alimkabidhi Site Mkandarasi M/S Dimetoclasa Real Hope Ltd kwa ajili ya kuanza ujenzi wa hospitali yenye hadhi ya rufaa kwa Tshs. Bilioni 25 katika hafla ya kusaini mkataba iliyofanyika kwenye kijiji cha Bulamba.

Leo tarehe 08 Februari, 2025 timu ya ufuatiliaji ujenzi wa hoapitali ya rufaa ya Mkoa imetinga site (Site meeting 2) kwa ajili ya kufuatilia ujenzi wa hospitali hiyo ili kujiridhisha na kasi ya ujenzi pamoja na utekelezaji wa makubaliano ya matakwa ya mkataba kwa masilahi ya wananchi wa kisiwani humo.

Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya miundombinu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mhandisi Chagu Ng'homa amesema mpango wa Serikali ni kuanza kutoa huduma za afya mara moja pindi tu mradi utapokamilika kwa sehemu hiyo ya kwanza na ndio maana ujenzi umejumuisha majengo muhimu.

Amesema, jengo la ghorofa lenye uwezo wa kubeba vitanda 180, jengo la kuhifadhia maiti, kazi za nje na jengo la umeme pamoja na ofisi za walinzi ni sehemu ya majengo ya awali kutekelezwa na kwamba ndani ya siku 545 (Miezi 18) yatakamilika na huduma zitaanza kutolewa mara moja.

Katika kuhakikisha kasi ya ujenzi inaongezeka, Mhandisi Chagu akiwa kwenye ukaguzi wa eneo la ujenzi amepiga simu ya moja kwa moja kwa Mhandisi wa Wakala ya Umeme vijijini (REA) na kumtaka afike kwenye eneo hilo ili kuona namna ya kupeleka mradi wa umeme kwa ajili ya utekelezaji wa mradi

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Jesca Lebba amesema sambamba na ujenzi huo taratibu zingine za kupata vifaa vya tiba na samani zinaendelea ili kuhakikisha mara tu ujenzi ukikamilika huduma za afya zinaanza kutolewa kwa wananchi wa Ukerewe.


Kwa upande wa mkandarasi, Mhandisi John Bhoke amesema shughuli za kuweka uzio kwenye eneo hilo zimekamilika, uondoaji wa udongo wa juu pamoja na kuandaa vipimo na eneo la jengo kuu la mradi zimeshakamilika na kwamba kwa sasa kazi inatakayofuata ni ujenzi wenyewe.

Aidha, ametoa wito kwa Mkandarasi mshauri pamoja na msimamizi wa mradi kuendelea kushirikiana na kuwasiliana mara kwa mara ili kupata uelewa wa pamoja wa kufanikisha ujenzi huo kwa ufanisi pamoja na kuhakikisha malipo hayachelewi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti