• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Tuendelee kuchukua tahadhari dhidi ya mlipuko wa Kipindupindu: Dkt.Rutachinzibwa

Posted on: January 20th, 2024
  • Tuendelee kuchukua tahadhari dhidi ya mlipuko wa Kipindupindu: Dkt.Rutachinzibwa


Leo Januari 20, 2024 Mganga mkuu wa mkoa wa Mwanza Dkt.Thomas Rutachunzibwa amekutana na makundi maalum kwa lengo la kuwapatia elimu na kuwataka kuchukua tahadhari zote dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu ikiwemo ulaji wa chakula cha mkusanyiko wa watu wengi.

Akizungumza nao kwenye ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa, amesema baadhi ya wagonjwa waliofuatiliwa walibainika kupata maambukizi hayo kutoka msibani hivyo ni vyema kuwa makini eneo hilo kwa kunawa maji yanayo tiririka na kuepuka kwa kipindi hiki kulala matanga.

"Ni lazima kila mmoja wetu atambue kilicho mbele yetu kwa sasa na tuzingatie usafi kwenye maeneo yanayo tuzunguka tukuzingatie yote haya visa vya mlipuko vitatoweka", amesisitiza Mganga Mkuu wa Mkoa.

Amesema tusiache jukumu hili kwa Serikali pekee bali kila mmoja awe makini na kutoa elimu hii kwa wengine ili jamii iendelee kubaki salama na kuendelea na majukumu ya  ujenzi wa Taifa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana aliyehitimisha mafunzo hayo mafupi ya utoaji elimu kwa makundi maalum amesema Kipindupindu kinapona endapo mgonjwa aliyebainika atafikishwa mapema kwenye vituo vya afya vilivyotengwa na matibabu yake ni Bure hivyo jamii yote izingatie miongozo yote ya tahadhari inayotolewa na wataalamu wa afya kwa lengo la kulinda nguvu kazi ya Taifa isipotee.

By

"Huu ni ugonjwa wa aibu yaani mtu kula kinyesi kibichi kinachotokea na vimelea,naamini mafunzo haya ya leo mliopatiwa yatakuja na matokeo chanya",Mkuu wa Wilaya Nyamagana.

Mratibu wa elimu ya afya kwa umna Mkoa wa Mwanza Leonald Mlyakado amebainisha Serikali inaendelea na zoezi la uelimishaji na kukagua maeneo yote yenye viashiria hatarishi na ugonjwa huo na kuchukua hatua za kitaalamu.

Mmoja wa wanufaika na elimu hiyo Alfred Kapore ameishukuru Serikali kwa utoaji wa mafunzo hayo kwani baadhi walikuwa hawana ufahamu wa kutosha kumtambua mgonjwa wa Kipindupindu na tahadhari nyingine.

Makundi hayo maalum yaliyonufaika na elimu hiyo ni walemavu,vijana,wanawake,wafanyabiashara wadogo na maafisa usafirishaji.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti