• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Tulilinde Ziwa Victoria ili litupe Matunda : Byabato

Posted on: September 26th, 2023

Tulilinde Ziwa Victoria ili litupe Matunda : Byabato


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Afrika  

Mashariki) Mhe. Steven Byabato leo Septemba 26, 2023 amefika Kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kufuatia ziara yake ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya kisekta mkoani humo.

Akiongoza ujumbe alioongozana nao kwenye mazungumzo na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Byabato ametoa wito kwa wadau kwenye ukanda huo kulilinda Ziwa Victoria kwa maslahi ya vizazi vya sasa na baadae.

Amesema ziwa hilo linalounganisha Mataifa mbalimbali Afrika kwa dahari ya miaka limekua likistawisha uchumi wa Utalii na ukuaji wa sekta ya uvuvi hususani kwa nchi za Afrika Mashariki hivyo kila mmoja anapaswa kulilinda lisiharibiwe wala kuchafuliwa.

Tunalilinda ziwa letu ili nalo litulinde sisi, sheria za usimamizi wa bonde la ziwa Victoria ni lazima zizingatiwe ili ziwa letu lilete matunda kwetu sio tu kwa usafirishaji na chakula bali hata kwa uchumi wa uvuvi na Utalii." Amesema Byabato.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi ametumia wasaa huo kumshukuru Mhe. Rais Samia kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati Mkoani humo huku akitolea mfano wa Daraja la Kigongo Busisi, Meli ya MV Mwanza, Machinjio ya Kisasa, miradi ya usafi wa mazingira pamoja na mradi wa Maji wa Butimba ambao uko mbioni kukamilika.

Mhe. Makilagi amefafanua kuwa miradi hiyo ni kielelezo kwamba Mhe. Rais Samia amekusudia kuwahudumia wananchi kwa kuwaondolea kero kwenye huduma za kijamii kwenye sekta za Miundombinu,  Maji, Afya, Kilimo, Usafi wa Mazingira na Elimu.

Ziara ya Mhe. Byabato Mkoani Mwanza imejikita kwenye ukaguzi wa miradi mbalimbali ukiwemo Mradi wa Usafi wa Mazingira Pasiasi unaosimamiwa na Bonde la ziwa Victoria ambapo atajionea hatua ya utekelezaji iliyofikiwa kwenye miradi hiyo muhimu kwa maendeleo ya Taifa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti