• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

TULINDENI NGUVU KAZI YA TAIFA KWA KUWACHANGIA FEDHA WATOTO WENYE SARATANI: RC MTANDA

Posted on: May 4th, 2024

TULINDENI NGUVU KAZI YA TAIFA KWA KUWACHANGIA FEDHA WATOTO WENYE SARATANI: RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda leo Mei 4, 2024 amezindua rasmi mbio za Bugando Health  Marathon zenye lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya matibabu kwa watoto wenye Saratani na wasio na uwezo wa kumudu matibabu hayo.

Akizungumza na washiriki wa mbio hizo kwenye Hospitali ya Bugando, Mtanda amezitaka Taasisi na wananchi wote watakaojaaliwa kuunga mkono zoezi hilo ili kulinda nguvu kazi ya Taifa.

"Awali ya yote niupongeze uongozi wa Hospitali ya Bugando chini ya Mkurugenzi wake Dkt. Fabian Masaga, kwa ubunifu huu wa kutafuta fedha kwa nia njema ya kuokoa vizazi vyetu,ni ukweli gharama ya matibabu ya Saratani ipo juu na wengi hatuwezi kuimudu," Mhe.Mtanda.

Mkuu huyo wa Mkoa aliyeshiriki mbio za km 5 amesema mpango huo umekuja wakati mwafaka hasa kutokana na idadi ya watoto wanaogundulika na Saratani kuongezeka kutoka 50 kwa mwaka hadi 300, hivyo jitihada kama hizo zinapaswa kuungwa mkono.

"Nimeguswa na zoezi hili la uchangiaji na Ofisi yangu inatoa shs milioni 5 nikiwa na imani wengi mtajitokeza ili kufaniikisha malengo ya kuwasaidia watoto hawa,"amesisitiza Mhe.Mtanda

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Bugando Dkt.Fabian Masaga amebainisha malengo ya mbio hizo za Marathon ni kupata zaidi ya shs bilioni moja zitakazowasaidia watoto wasio na uwezo,malengo mengine ni kuhamasisha jamii kujenga tabia ya kuchangia,kuhimiza kushiriki michezo na kufahamiana kwa ujumla.

"Ada ya ushiriki wa mbio hizi ni shs 35,000 na tutakuwa tukifanya mazoezi haya kila Jumanne na Ijumaa kabla ya kilele chake Agosti mwaka huu ambapo Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dotto Biteko atakuwa mgeni rasmi,"Dkt.Masaga

"Ugonjwa huu unatibika endapo mtoto ataletwa mapema Hospitali,changamoto ipo kwa baadhi ya wazazi kuanza kukimbilia tiba mbadala na baadaye kuja Hospitali wakati tayari ugonjwa umepiga hatua kubwa,"Dkt.Yoronimo Kashaigili,bingwa wa ugonjwa wa Saratani kwa watoto.

Kauli mbiu ya mbio za Bugando Health Marathon inasema,Kimbia,changia watoto wenye Saratani.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti