• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Tumieni fursa zilizopo Mwanza kutanua wigo wa kazi zenu za usindikaji maziwa-RAS Balandya

Posted on: September 26th, 2023

Tumieni fursa zilizopo Mwanza kutanua wigo wa kazi zenu za usindikaji maziwa-RAS Balandya


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg.Balandya Elikana amewashauri wasindikaji wa maziwa kutumia fursa zilizopo Mkoani humo ili kutanua wigo wa kazi zao ili wazidi kujiimarisha kiuchumi na kujihakikishia pato lao.

Akifungua kongamano la wadau wa tasnia ya maziwa kwa niaba yake, leo septemba 26, 2023 kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya uchumi na uzalishaji,Emil Kasagara amesema fursa za reli ya kisasa inayotarajiwa kukamilika mwakani, mgodi wa Nyanzaga na Daraja la JP Magufuli ni eneo ambalo ni mkombozi kwa wasindikaji kufanya kazi zao kwa uhakika.

"Ndugu zangu wadau mliohudhuria kongamano hili, sasa muanze kuangalia hatua ya kuwa na viwanda kutokana na uhitaji wa mzigo mkubwa kupita fursa zilizopo Mkoani Mwanza mkizingatia uzalishaji ulio bora ili muweze kumudu soko la ushindani",amesisitiza Kasagara.

Amesema kuna asilimia asilimia 30 ya hali ya udumavu kwa watoto wetu kutokana na ukosefu wa unywaji wa maziwa hali inayochangiwa na kushindwa kumudu vizuri masomo yao,hivyo kupitia jukwaa hilo la kongamano waje na matokeo chanya katika kuleta mapinduzi ya hali ya unywaji wa maziwa shuleni.

Awali akizungumzia lengo la kongamano hilo kuelekea kilele cha siku ya unyweshaji maziwa shuleni yanayofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza,Msajili kutoka Bodi ya maziwa Tanzania TDB,George Msalia amebainisha wamekutana na wadau hao ili kubadishana uzoefu na kubaini changamoto zao ili kuzifanyia kazi na mwishowe kuwepo na tija katika unywaji wa maziwa shuleni.

"Hapa tuna wataalamu mbalimbali watakaowasilisha mada zikiwemo Taasisi za Fedha hasa kwa kutambua changamoto za mitaji kwa kutambua ni bidhaa inayohitaji mazingira safi na umakini usipokuwepo hasara ya kuharibika kwa haraka inajitokeza hivyo huduma za kibenki zina nafasi yake",Msalia.

"Hadi sasa tuna mikoa 8 inayotekelezwa mpango huu wa unyweshaji maziwa shuleni na tuna shule 134 mpango ni kufikia shule 5000," amefafanua Prof.Zacharia Masanyiwa Mwenyekiti wa Bodi ya maziwa Tanzania TDB

Kongamano hilo limewakutanisha pia walimu wa kutoka shule za Msingi na Sekondari ambapo mpango wa unyweshaji maziwa unatekelezwa shuleni kwao.

Aidha katika kuelekea kilele cha maadhimisho hayo wadau wa tasnia ya maziwa walitembelea shule kadhaa Mkoani Mwanza kutoka Wilaya za Nyamagana na Ilemela na kugawa maziwa kwa wanafunzi pamoja na kutoa elimu kuhusu umuhimu wa unywaji maziwa.

Kila Jumatano ya mwisho wa mwezi wa Septemba Tanzania inaungana na Mataifa mengine Duniani kuadhimisha siku ya unyweshaji maziwa shuleni ambapo Kitaifa mwaka huu yanafanyika Mkoani Mwanza Septemba 27,2023 kwenye viwanja vya Furahisha.

Kauli mbiu ya mwaka huu inasema "MPE MTOTO MAZIWA KWA MAENDELEO BORA SHULENI".

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti