• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Tumieni vikao vya Mabaraza Kuzalisha Takwimu sahihi kwa faida ya Taifa: RAS Mwanza

Posted on: December 20th, 2023

Tumieni vikao vya Mabaraza Kuzalisha Takwimu sahihi kwa faida ya Taifa: RAS Mwanza


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndg. Elikana Balandya leo Disemba 20, 2023 amefungua kikao cha tano cha Baraza la sita la wafanyakazi wa ofisi ya Taifa ya Takwimu na kuwataka kutumia vizuri jukwaa hilo kuzalisha Takwimu bora itakayoleta  Maendeleo kwa Taifa.

Akizungumza na wajumbe wa Baraza hilo kwenye ukumbi wa mikutano Rock City Mall,Balandya amebainisha baraza hilo lina wajibu wa kujenga uelewa wa pamoja wa masuala mbalimbali ya Taasisi na kuhimiza nidhamu kwa upana wake, yote hayo yakifanyika kwa ukamilifu Serikali itaweza kupanga mipango yake ya maendeleo itakayokuwa na tija kwa wananchi.

"Ndugu wajumbe NBS ina jukumu la msingi la kuhakikisha takwimu zinazozalishwa nchini kwa matumizi mbalimbali zinakuwa bora,hivyo baraza hili litasimama kuwa chombo cha kufanya tathmini majukumu mbalimbali yanavyotekelezwa kwa ufanisi,"amefafanua Mtendaji huyo wa Mkoa wakati anazungumza na wajumbe wa baraza hilo wanalokutana kwa siku mbili.

Amewapongeza makamisaa wa Sensa ya watu na makazi 2022,Mhe Anne Makinda kutoka Bara na Mhe.Balozi Mohamed Hamza wa Zanzibar  kwa kusimamia vizuri zoezi la Sensa  iliyofanyika mwaka 2022 ambayo ilikuwa bora.

"Tunamshukuru Rais wetu Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa mafanikio ya Sensa hiyo ambayo ilifanyika katika mazingira ya kisasa ambapo sasa tunawarudishia matokeo yake wananchi kwa kuwaelimisha mipango mbalimbali ya kimaendeleo,"Mhe.Anne Makinda,Kamisaa wa Sensa 2022

Mtakwimu Mkuu wa Serikali Bi.Albina Chuwa amebainisha Sensa ya watu na makazi 2022 ilikuwa ni miongoni mwa Sensa bora ulimwenguni kutokana na kuwa na miundombinu ya kisasa hali iliyoleta ufanisi wa kazi wakati wa zoezi hilo.

Awali kabla ya kwenda kufungua kikao hicho Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza,Ndg.Balandya Elikana mapema asubuhi aliupokea ugeni Ofisini kwake uliofika kujitambulisha na mazungumzo mafupi ukiongozwa na makamisaa wa Sensa ya watu na makazi 2022, Mhe.Anna Makinda wa Tanzania Bara na Mhe.Balozi Mohamed Hamza kutoka Zanzibar.

Katika mazungumzo hayo Balandya amesema hali ya usalama Mwanza ni shwari na mvua zinazoendelea kuonyesha hazijaleta madhara makubwa gkulinganisha na mikoa mingine zaidi ya mafuriko ya muda mfupi kwa waliojenga kwenye njia za asili za maji.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti