• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

UFUGAJI WA KISASA WA SAMAKI UTAONGEZA TIJA KWA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI :NAIBU WAZIRI

Posted on: August 13th, 2024

UFUGAJI WA KISASA WA SAMAKI UTAONGEZA TIJA KWA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI :NAIBU WAZIRI


Mkutano wa tatu wa ukuzaji viumbe maji Afrika Mashariki umefunguliwa rasmi leo Agosti 13, 2024 Jijini Mwanza na rai imetolewa ya kutolewa kwa elimu ya ufungaji wa kisasa wa samaki kwa njia ya vizimba.

Akifungua mkutano huo, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe.Alexander Mnyeti amesema uvuaji holela umepitwa na wakati na umesababisha samaki wengi kupotea wakiwemo Ningu na Gobogobo.

Mnyeti amebainisha kuwa licha ya ziwa hilo sehemu kubwa kuwa Tanzania lakini bado hatujalitumia vizuri kulinganisha na wenzetu wa nchi jirani kama Uganda.

"Huku kwetu tuna jumla ya vizimba 168 hivi kwenye ziwa Victoria na Tanganyika lakini Uganda wao wana vizimba zaidi ya 2000, hapa tunaona bado tunahitaji mkazo wa kuelimishana", Mhe. Mnyeti.

Amesema, Serikali imeweka mazingira mazuri katika sekta ya uvuvi kwa kutoa fursa za mikopo bila riba kutoka benki ya TADB lengo likiwa ni kufanya shughuli hiyo kwa tija.

Amezitaka pia taasisi zinazojihusisha na maendeleo ya ziwa Victoria kuzidi kubuni mikakati ya kuwalinda viumbe maji kwa kulipumzisha ziwa hilo na shughuli za uvuvi.

Akitoa salamu fupi za Mkoa wa Mwanza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe. Hassan Masalla ameishukuru Serikali ya Rais Samia kwa kuzidi kuiboresha sekta ya uvuvi na ajira kwa ujumla.

"Zaidi ya Tshs bilioni tano zimeletwa Mwanza, boti 26 za kisasa pamoja na vizimba 16, hii imechangia kuongeza tija katika sekta hiyo", ameeleza Mhe.Masalla.

Jumla ya Mataifa 18 yanashiriki mkutano huo zikiwemo Uganda, Kenya, Malawi, Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo pamoja na Nigeria.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti