• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

UKWEPAJI KULIPA KODI NI UKATILI UNALENGA KUUA UCHUMI WETU - RC MTANDA.

Posted on: February 20th, 2025

UKWEPAJI KULIPA KODI NI UKATILI UNALENGA KUUA UCHUMI WETU - RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa rai kwa Viongozi wa Taasisi za Umma na zisizo za umma kuendelea kuwa mabalozi wazuri katika kulipa kodi na kuhimiza watumishi walio chini yao kidai risiti wakati wote wanapofanya manunuzi ya bidhaa au huduma ili tujenge uchumi wa nchi.

Mkuu wa Mkoa ametoa kauli hiyo usiku wa leo Februari 19, 2025, alipokuwa akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mlipa kodi iliyofanyika katika Ukumbi wa Rock City Mall, Ilemela na kuupongeza uongozi mzima wa TRA kwa kuja na wazo hilo la namna ya kipekee kabisa la kuwashukuru walipakodi.

Aidha, Mhe. Mtanda ametoa rai kwa kila mmoja kuhakikisha analipa kodi sahihi na kwa hiari kwani kodi hizi ndio zinarudi tena kwetu katika mfumo wa huduma mbalimbali ambazo serikali inazitoa kwa wananchi wake.

“Sambamba na hilo niwakumbushe Mamlaka ya Mapato Tanzania kuendelea kutoa elimu ya kodi kwa wananchi ili kila mmoja aweze kutekeleza wajibu wake jinsi inavyompasa”.

Sambamba na hayo Mhe. Mtanda amewapongeza walipakodi wote waliopongezwa kwa kulipa kodi zao vyema na amewasihi zawadi hizo walizopewa kuwa chachu kwao na kwa wengine wengi kujifunza ya kwamba kodi ni jambo la kizalendo na linahitaji ushirikiano wa pamoja kati ya serikali na wananchi wake ili kuiwezesha nchi kupiga hatua zaidi na zaidi.

Naye Bw. Faustine Mdessa, Meneja wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Mwanza, amesema ujio wa wazo hilo inadhihirisha kwamba TRA inathamini mchango

wa walipakodi katika makusanyo ya mapato ambayo yanaiwezesha serikali kutekeleza mambo mbalimbali yakiwemo kuboresha huduma za afya, ulinzi na usalama wa nchi.

Kadhalika amesema kuna kuna baadhi ya wafanyabiashara wanakosa uaminifu na kuwarubuni wateja kwa kuwashushia bei za bidhaa na huduma ili kuwapa risiti za bei ambazo sio sahihi hali inayopelekea mapato mengi kupotea.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti